26th November 2011
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Awali, wafanyabiashara walikuwa
wakilalamikia hatua ya TRA kuwatoza ushuru wanaponunua bidhaa Zanzibar
na pia zinapofika Tanzania Bara zinatozwa tena.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam,
na Ofisa Mkuu wa Elimu kwa Walipa Kodi Kanda ya Mashariki, Hamisi
Lupenja, alipozungumza na waandishi wa habari.
Lupenja alisema ushuru huo uliondolewa
kufuatia mapendekezo ya kamati maalum iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete,
kwa ajili ya kushughulikia kero za Muungano.
Alisema hivi sasa ushuru unalipwa kwa
upande mmoja tu wa Muungano kwa bidhaa mbalimbali tofauti na ilivyokuwa
siku za nyuma, ambapo mfanyabiashara alikuwa akilipa Zanzibar na akifika
Tanzania Bara analipa tena.
Lupenja alisema mpango huo umekwisha
kuanza ingawa hakusema ulianza lini, lakini alikiri kuwa kwa sasa kuna
unafuu kwa wafanyabiashara wa pande mbili za Muungano.
Wakati huo huo, TRA imeanzisha mpango wa
kutoa elimu kwa wafanyabiashara wenye ulemavu wa kuona (vipofu), kwa
lengo la kuongeza wigo wa ulipaji kodi kwa hiari.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment