Friday 11 November 2011

MLANGO ULE ULE ZANZIBAR ILIPITITISHWA KUJITOA JUMUIYA YA KIISLAMU (IOC) NDIO HUO HUO WA KUINGILIA FIFA:



Na Ramadhan Ali

Zanzibar ikiwa ni Nchi ya Kiislamu, ilishurutishwa Enzi za Utawala wa Rais Mwinyi na  Dr.Salmin,miaka ya 1990, kujitoa kutoka Jumuiya  ya Nchi za Kiislamu (IOC) kwa kuwa  swali la uwanachama  ni la Muungano- swali la siasa ya nje ya Tanzania.
Jaribio jengine la Zanzibar au  Zanzibar Football Association (ZFA) kujiunga  na International Federation of Football Associations (FIFA) lilikataliwa  mwaka huu.  Hoja : eti "Zanzibar si nchi" na hivyo haina " Mamlaka "  (Sovereignity) kukubalika kuwa Mwanachama wa FIFA kinyume na England,Wales,Scotland na Ireland ya Kaskazini.(Special status)eti kwa kuwa England ndie mama wa dimba-mother of football.

Lakini, ikiwa kujiunga nchi ya kiislamu ya Zanzibar- (Mecca ya Afrika Mashariki ) katika Jumuiya ya Kiislamu, ni mwiko kwasababu Zanzibar haina Mamlaka hayo na imejiingiza IOC kwa mlango wa nyuma, WAKATI  sasa  UMEWADIA kwa WAZIRI WA  MICHEZO wa Zanzibar Bw.Jihad, Baraza la Taifa la Michezo la Zanzibar  na Uongozi wa ZFA kuvaa njuga na  kuanza  KUHOJI  Tanzania-bara ilijiunga vipi na FIFA;Halmashauri Kuu ya Olimpik Ulimwenguni (IOC) kupitia  Tanzania Olimpic  Committee (TOC),Shirika la Mabondia Ulimwenguni na Mashirika mengine ya KIMATAIFA  wakati "MIMICHEZO" au "SPOTI" si swali la MUUNGANO  kama wenzao Tanzania-bara walivyohoji uwanachama wa Zanzibar katika IOC ?.

JE,MASHIRIKA YA SPOTI YA PANDE HIZO MBILI YALIKAA PAMOJA NA KUOMBA UWANACHAMA KWA UBIA ?

Alao katika Shirikisho la dimba Ulimwenguni FIFA, hali haioneshi kuwa hivyo.Laiti ingelikuwa hivyo,  ZFA isinge hanikiza kupiga  hodi mlangoni mwa FIFA kuomba uwanachama wake pekee.  Mabaraza 2 ya Taifa ya Spoti ya pande hizo mbili  sasa yanapaswa kuitisha kikao kujadili  NANI mwenye MAMLAKA hasa ya  KUIWAKILISHA  TANZANIA  KIHALALI katika Mashirika ya Spoti ya Kimataifa mfano wa  FIFA,IOC na World Boxing Federation, nikitaja Mashirika machache tu ya Kimataifa  wakati SPOTI si swali la Muungano.

Wakati muwafaka    kutafuta UFUMBUZI wa MEDANI YA SPOTI kwa Nchi mbili za Tanzania   ni  huu -sasa inapojadailiwa KATIBA MPYA.
Dimba linapaswa kwanza kuchezwa nyumbani Dar-es-salaam na Zanzibar kabla kukimbilia Zurich-Makao Makuu ya FIFA , Cairo-Makao Makuu ya CAF-Shirikisho la Kabumbu la Afrika au Lausane,Uswisi,Makao Makuu ya Kamati ya Olimpik Ulimwenguni. Pande hizo 2 zikae kutatua kero hii nyengine ya Muungano.
Katika Vikao hivyo vya serikali hizo mbili na Mabaraza  2 ya Michezo ya Kitaifa,kuna KITANDAWILI kinachobidi kufumbuliwa:

ILIKUAJE   Tanganyika kwa  kutumia KAWA la Tanzania , inaendelea kubeba BENDERA ya Tanzania medani za Kimataifa ilihali SPOTI si  SWALI LA MUUNGANO ?

Hapa Serikali ya SMZ,ZFA na Baraza la Michezo la Zanzibar, ina turufu  nzito ya kuwafanya ndugu zao wa Tanzania-bara  kuridhia kukaa pamoja nao  tena kwa nia safi kuchanganya upya karata na kuamua :

1.Ama kuacha Spoti kuendelea kuwa swali si la Muungano na kila moja isake uwanachama wake ulimwenguni au
2. kubadili Katiba /Hati ya Muungano na kulijumuisha katika Orodha ya Maswali ya Muungano na kuwa na timu moja.

Zanzibar ishikilie TANZANIA-BARA iache  kupepea BENDERA ya Tanzania katika medani za Kimataifa ilhali  swali  la  spoti  si  la Muungano.
Tanzania ni Muungano wa Nchi 2 na hakuna Upande wenye haki kulitumia jina  hilo kwa masilahi ya Upande mmoja tu katika maswali  yasio ya Muungano.
Ni hapa inapostahiku kuhoji TANZANIA katika FIFA/IOC/WBF na kadhalika,  inamuakilisha nani-Tanganyika au Zanzibar ?
Nani katoa Mamlaka  au Idhini ya Uwaklilishi huo ?

JE,MASHIRIKA HAYO YA KIMATAIFA YALIFICHWA KUWA SPOTI SI SWALI LA MUUNGANO  AU YALIZIBWA  MACHO  KUSUDI?
 KWANINI FIFA ILIPOUKATAA UWANACHAMA WA ZFA HAIKUHOJI UWANACHAMA WA TFF CHINI YA MISINGI SPOTI SI SWALI LA MUUNGANO ?
KWANINI UOGOZI WA ZFA HAUKOHOJI UWANACHAMA WA TFF  AU HAIKUA DIPLOMASIA  MURWA?
IKIWA NI HIVYO,
MBONA WENZAO WALIHOJI UWANACHAMA WA ZANZIBAR KATIKA IOC-JUMUIYA YA KIISLAMU NA KUIVUA NGUO ZANZIBAR HADHARANI ITOKE ? KWANINI MARAIS WAO WALIFEDHEHESHWA :MZEE MWINYI NA KOMANDOO ? JE, WALIOWADHIRI Hawakujua Diplomasia au kutambua  ukweli kuwa 99% ya Wazanzibari ni waislamu nawangefaidika  kimisaada ?

Ikija ikadhihirika kuwa  Mashirika ya Spoti ya Tanzania-bara yameingia katika Vyama na Jumuiya za Kimataifa kinyemela kama ilivyoingia Zanzibar katika Jumuiya ya Kiislamu miaka ya 1990   mlango wa nyuma na kulazimishwa ITOKE, Tanzania inabidi kUSIMAMISHWA UWANACHAMA WAKE hadi kwanza swali la UHALALI wa UWAKILISHI WAKE liempatiwa ufumbuzi na pande zote mbili baada ya kuamua hadhi (Status ) ya michezo katika Muungano.


Kwahivyo, MLANGO ULE ULE ZANZIBAR ILIOTOLEWA NJE YA JUMUIYA YA NCHI ZA KIISLAMU (IOC), NDIO UWE  ULE ULE  ZFA WA KUINGILIA FIFA .
Ama sivyo, pande zote 2 za Tanzania,  zifunge virago na zikae nje  ya FIFA/ Kamati ya Olimpik Ulimwenguni (IOC) na Mashirika mengine ya Kimataifa kama  zilivyokaa nje ya Jumuiya ya Kiislamu (IOC) zote mbili  tangu enzi za Utawala wa Rais Mwinyi na Dr.Salmin pale KIBIRITI kilipotikiswa huko Dodoma.
Wakati kukaa nje ya Jumuiya ya Kiislamu hakutawakera baadhi ya  Watanzania-bara wasiowaislamu ,kukaa nje ya  FIFA , CAF ,Michezo ya Olimpik (IOC) kutawakereketa  wote bila ya kuchagua dini au madhehebu na hivyo, watatafuta haraka UFUMBUZI   kukitegua KITANDAWILI-TEGA.Ufumbuzi huo uje tena kabla ya Kombe la Dunia la FIFA 2014 na Michezo ya OLimpik Brazil,2016.
Mpira  sasa uko langoni  mwenu Wazanzibari muucheza. Wenzetu wameshatia goli langoni mwa FIFA/IOC/World Boxing Federation na Mashirika mengine ya Kimataifa.
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Ramadhan Ali is the Author of "Africa at the Olympics, "The Rise of African Football,1984" and "African football Stars in the Bundesliga,2002"

1 comment:

  1. It is high time now kwa wazanzibari kusema enough is enough kwa so called Muungano. kila kitu kina wezekana kinachotakiwa ni kujipanga tu na kujua tunataka nini. kwa nini sisi wazanzibari tumekuwa wanyonge sana kiasi hichi wanachoaamua watanganyika sisi twakubali tu why tunaogopa kusema, viongozi wetu munatupeleka wapi. nadhani sasa hivi sio wakati wa kutegemea viongozi ni wakati sasa kwa wananchi wote wanaoipenda zanzibar kujitolea kwa nguvu zao zote kuipigani zanzibar kutoka katika mikono ya kidhalimu ya mkoloni Tanganyika. Tukiamua tunaweza ....

    ReplyDelete