Friday, November 11, 2011
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, ameondoka nchini jana
kuelekea Falme za Kiarabu kwa ziara ya wiki moja.
Katika ziara Dk. Shein
amefuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein, waziri wa Kazi Uwezeshaji
Wananchi Kiuchumi na Ushirika, Haroun Ali Suleiman na waziri wa
Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui.
Wengine alioambatana nao ni Naibu
waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mahadhi Juma Maalim, Mshauri wa Rais Uhusiano wa
Kimataifa na Uwekezaji Balozi Mohammed Ramia, Mkurugenzi Mtendaji
Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar, Salum Khamis Nassor pamoja
na watendaji wengine wa serikali.
Akiwa nchini humo, Dk. Shein anatarajia kukutana na viongozi mbali mbali pamoja na wafanyabiashara, wenye viwanda na wawekezaji.
Miongoni mwa viongozi
atakaokutana nao ni kiongozi wa Ras-Al-Khaiman Sheikh Saud bin Saqr
Al-Qasimi, kiongozi wa Sharjah Sheikh Sultan Mohammed Al-Qasimi na
viongozi wengineo.
Aidha, Dk. Shein atatembelea maeneo mbali mbali ya viwanda, bandari pamoja na maeneo ya kihistoria.
Chanzo: ZanziNews
No comments:
Post a Comment