Monday 31 December 2012

Ghana yapiga marufuku majokofu mitumba

Serikali ya Ghana imepiga marufuku uagizaji wa majokofu yaliyotumika au mitumba ili kupunguza matumizi ya nishati na uchafuzi wa mazingara.
Majokofu mengi kukuu yana kemikali inayoitwa Chlorofluorocarbons (CFCs) inayoharibu mazingiria.
Licha ya kuwa bidhaa hizo zimepigwa marufuku, na hazitengenezwi tena, majokofu hayo yanaaminika kutumika barani Afrika.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Nishati ya Ghana ameimbia BBC kuwa marufuku hiyo, imelifanya taifa lao kuwa kielelezo katika kanda ya Afrika Magharibi.
Sheria ya kupiga marufuku majokofu hayo iliidhinishwa mwaka wa 2008, lakini muda wake uliongezwa ili kuwa na wauzaji wa bidhaa hizo kufanya marekebisho.
Hata hivyo wafanyabiashara kadha nchini Ghana wameshutumu uamuzi huo wa serikali wakisema idadi kubwa ya watu watakosa kazi.
Afisa mkuu wa tume hiyo ya nishati Alfred Ofosu-Ahenkora amesema majokofu hayo ya mitumba yanaharibu taifa hilo kwa sababu hayakutengenezwa kutumika barani Afrika na pia yanatumia kiasi kikubwa cha umeme.

Sababu ya kuyapiga marufuku

Tume hiyo imesema zaidi ya majokofu milioni mbili zilizoagizwa kutoka ng'ambo hususan kutoka mataifa ya Ulaya.
Kemikali za CFCs zimepigwa marufuku kwa mujibu wa azimio lililotiwa saini mjini Montreal Canada, kuzuia kemikali zinazoharibu tabaka la hewa ya Ozone.
Ili kuhimiza raia wa nchi hiyo kutotumia majokofu hayo, serikali imetoa ruzuku kwa kuwapa majokofu mapya wanaorudisha ya zamani.
Mwandishi wa BBC mjini Accra anasema, sio raia wengi wa taifa hilo wanaweza kumudu gharama ya jokofu jipya, kwa hivyo mahitaji ya majokofu ya mitumba yamekuwa makubwa, katika maduka yanayouza bidhaa hiyo katika mji mkuu wa nchi hiyo.
'' Tutapoteza kazi yetu mwaka ujao, hii ndio biashara inayotupa sisi fedha za kulisha familia zetu'' alisema mmoja wa wafanyabiashara Albert Kwasi Breku.
Lakini Bwana Ofosu-Ahenkora amesema suluhisho la kudumu ni kuanzisha kiwanda cha kutengeneza majokofu nchini humo.
'' Suala la kufunga biashara za watu sio wazo zuri, ila serikali ingeliimarisha kwa kuanzisha viwanda zaidi na nadhani hilo litasaidia kubuni nafasi zaidi za kazi, badala ya kuagiza majokofu ya mitumba'' alisema Ahenkora.
Tangu kemikali ya CFCs, kupigwa marufuku, kampuni nyingi za kutengeneza majokofu zimekuwa zikitumia ina mpya inayoitwa Hydrofluorocarbons (HFCs).
Lakini mwaka uliopita ripoti ya Umoja wa Mataifa ilisema kuwa majokofu yanayotumia mfumo huo mpya wa HFCs yanatoa hewa ya sumu zaidi ambayo ni asilimia ishirini hatari zaidi kuliko hewa ya Carbon Monoxide au CO2, na hivyo matumizi ya teknolojia hiyo huenda yakaathiri mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Taifa la Ghana katika miaka ya hivi karibuni limekuwa kivutio cha mabaki ya viwanda vya kompyuta na televisheni kutoka mataifa ya Magharibi, na nyingi kati ya mabaki hayo yana sumu.
Chanzo: BBC

Wednesday 26 December 2012

Jinsi watawala wanavyowatumia wasomi wetu

Barazani kwa Ahmed Rajab
TAKRIBAN nchi zote za Kiafrika zimeshuhudia jinsi baadhi ya raia wake walivyojilimbikizia utajiri mkubwa na fedha nyingi mno wakiwa katika vivuli vya utawala. Baadhi yao ni watawala wenyewe.
Wengine wanawatumia hao watawala au mfumo uliopo wa utawala kujipatia mali hizo. Mara zote njia wanazozitumia huwa si za halali.
Hali hiyo haikuanza leo wala jana barani Afrika. Ibn Khaldun aliyefariki dunia 1406 aliyaona hayo zama zake. Bwana huyo alizaliwa Tunis na mababu zake walitokea Hadhramaut, Yemen Kusini.
Miongoni mwa fani alizosomea utotoni mwake ni isimu ya lugha ya Kiarabu, hisabati, mantiki na falsafa. Aliandika kitabu chake cha mwanzo akiwa na umri wa miaka 19. Ibn Khaldun anatambuliwa kuwa ndiye baba wa uandishi wa historia, wa elimu-jamii (sosiolojia) na wa sayansi ya uchumi.
Baada ya kuipata taalimu yote aliyojaaliwa kuipata Ibn Khaldun alifanya kazi serikalini akishika nyadhifa kadhaa za kisiasa pamoja na uwaziri. Wakati mmoja alikorofishana na mtawala Ibn Amar Abdullah na akaamua kuhama Tunis na kwenda Granada, Hispania, ambako alishika nyadhifa kubwa kubwa chini ya Sultan Muhammed wa tano. Siku hizo Hispania ilikuwa dola ya Kiislamu. Baadaye Sultani alimrejesha kwao Ibn Khaldun baada ya kuzuka uhasama baina ya waziri wake mmoja na Ibn Khaldun.
Aliporudi Afrika Ibn Khaldun alikaribishwa kwa mikono miwili na mtawala na akateuliwa waziri mkuu. Kutokana na muda wake mrefu katika duru za watawala Ibn Khaldun aliona mengi. Moja aliloliona na kulitaja ni kwamba ufisadi na udikteta ni pacha.
Na si lazima pawepo ufisadi wa kupora mali. Wanachofanya madikteta wengine — na huo pia ni aina ya ufisadi — ni kuwatunukia akina ‘hewalla bwana’ vyeo vikubwa wasivyostahili na mishahara minene au manufaa na marupurupu mengine.
Wanapoonyesha dalili ya kwenda kinyume na mtawala au hata pale mtawala anapokuwa na shaka nao basi vibarakala akina ‘hewalla bwana’ hupokonywa ulwa waliotunukiwa.
Katika mfumo huo mtawala analazimika kila mara kuwa na kitu cha kuwapa vibarakala au hata kuwapokonya walicho nacho ili hao watawala waweze kuidhibiti dunia yao.
Ufisadi wa aina hiyo hutokea hata katika nchi za kidemokarasia. Hivyo, si ajabu kwamba ufisadi wa aina zote umekithiri katika nchi zetu tangu wimbi la demokrasia lianze kung’uruma barani Afrika. Hii leo takriban kila nchi inaiigiza kivyake dhana hiyo.
Juu ya hayo si nyingi ya nchi za Kiafrika zilizo na mfumo wa demokrasia iliyokomaa. Nchi nyingine zimekuwa zikijitia tu katika mkumbo wa demokrasia kwa vile zilikuwa hazina hila ila kujifanya kuukubali mfumo huo. Ziliukubali shingo upande mfumo huo kutokana na mashinikizo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.
Kuna wenye kuipima demokrasia kwa kigezo cha uchaguzi lakini hicho ni kigezo kimoja tu. Tena kina mushkili wake kwani hata hicho kinatakiwa kiwe na sifa fulani. Kati ya sifa hizo ni kwamba uchaguzi uwe huru, wa haki, uliofanywa kwa uwazi kabisa na uwe wa kuaminika na wenye matokeo yasiokanika.
Ikiwa tutakitumia kigezo hicho cha uchaguzi na sifa hizo tulizozitaja basi ni nchi chache za Kiafrika zinazostahiki kuitwa za demokrasia halisi.
Katika miaka toka ya 1960 hadi 1990 mtindo uliokuwapo ni kwa serikali za Kiafrika kubadilishwa kwa njia ya mapinduzi ambayo mara nyingi yaliwaua viongozi. Baada ya muda walioua nao pia wakiuawa kwani kulikuwa hakuna mfumo mbadala wa kubadilishana madaraka.
Mtindo huo wa kupinduana haukuwa ukiendeshwa na wanakwaya wa kanisani. Ulikuwa ni mfumo wa kikatili ulioendeshwa na makatili.
Mtindo huo uligeuka na kuwa kama mila ya Afrika. ‘Udikteta wa Kiafrika’ ukawa unatumia mantiki ya kikatili na ya umwagaji damu. Lakini kila pale demokrasia ilipotia mizizi medani huwa si tena uwanja wa kunyakua madaraka.
Siku hizi kwingi Afrika madaraka hupatikana kwa yaliyomo kwenye madebe au visanduku vya kura na si kwa mtutu wa bunduki. Na Afrika hatuna upungufu wa visanduku vya kura. Taksiri iliyopo ni kwamba visanduku hivyo huwa ama vimekwishajazwa kura kabla ya wapiga kura kutumbukiza kura zao au hujazwa baadaye kwa kura za bandia. Hapo ndipo penye tatizo. Hapo ndipo tunapoweza kutofautisha baina ya demokrasia halisi na ile ya shaghalabaghala.
Kwa hivyo haitoshi nchi kujinata kwamba inafuata demokrasia. Katiba za nchi nyingi za Kiafrika zinasema kwamba zinaufuata mfumo huo. Lakini katika nchi hizo kuna pengo kubwa baina ya nadharia na vitendo, baina ya kilichomo ndani ya katiba na kinachotendwa na serikali na wakubwa wake.
Katika nyingi ya nchi za Kiafrika demokrasia imegeuzwa na kuwa tamthilia. Na sisi raia tumekuwa waigizaji wa tamthilia ya kidemokrasi. Watawala wetu ni wasanii mahiri. Wametuwekea majukwaa na yote yanayohitajika katika majukwaa hayo pamoja na maneno yote ya Kimagharibi yanayohitajika katika tamthilia hiyo pamoja na wahka na hali ya mshawasha inayozuka wakati wa kuhisabiwa kura.
Sisi tumezoea kuhamaki magazeti ya nchi za Magharibi yanapozielezea chaguzi zetu kuwa kama soko linalofunguliwa katika vipindi maalumu aghalabu vya miaka mitano mitano.
Pengine magazeti hayo yanasema kweli kwani chaguzi katika baadhi ya nchi zetu ni mzaha na viongozi wetu ni machale. Wakati mwingine chaguzi zetu zinakuwa mithili ya dansi kubwa ya vinyago. Ngoma inapomalizika visanduku vya kura hujazwa kura ambazo hakuna aliyezipiga.
Katika nchi zinazofanya uchaguzi wa bandia serikali huwa na uwezo wa kuwakashifu wasomi kwa kuwafanya wayakubali matokeo ya uchaguzi na hata kuwafanya wayathibitishe hadharani matokeo hayo. Hivyo wasomi hao hulainishwa laisa kiasi. Makali yao ya kuusema ukweli yanazimuliwa, wanageuzwa vibarakala na inapohitajika huhongwa marupurupu ya utawala
Chanzo: Raia Mwema

Saturday 22 December 2012

Wazanzibari tunayajuwa haya???


The Partnership
Na Aboud Jumbe
"Njia haikuwa rahisi na siku zote iliibuka ile shaka ya Zanzibar kumezwa na Tanganyika kwa kupitia Muungano huo. Kama vile Mwalimu alivyoonesha katika hotuba yake ya Sherehe za miaka 10 ya Muungano kuwa watu walikuwa na wasiwasi na "nchi ndogo kama Zanzibar kumezwa na nchi kubwa kama Tanganyika". Khofu hii haikuwa kwa watu wa Zanzibar tu. Kwa wafuatiliaji wengi hali hii ya zimwi kushirikiana na kibushuti kumeifanya dunia siku zote ikae ikisubiri ni kipi kitatokea. Picha inayoonekana ukitizama kipindi cha miaka thelathini ya Muungano huu ni ya kutisha. Inatia mashaka na masuali juu ya yale madhumuni halisi ya Muungano huu huku kukiwa kuna dalili za wazi za kukimbia matakwa ya Mkataba wa Muungano.

Inaweza kuwa jambo jema iwapo tutajiuliza: Kwa nini hapo 1963 nchi za Afrika Mashariki zilikuwa zimejifunga kukubali kuunda Shirikisho zikashindwa kujiunga na Muungano wa Tanzania? Hakuna moja iliyofanya hivyo. Jee, hii ni kutokana na mtiririko wa matukio kuanzia Aprili, 1964 kushindwa mbali ya kudhihirisha khofu ya kumezwa.
Ingefaa hapa nitaje kuwa miezi minne tu baada ya Muungano, marehemu Jomo Kenyatta alinukuliwa na gazeti la Times of London hapo Agosti 3, 1964 akisema hayuko tayari kumpigia magoti Nyerere na Tanganyika. Kitu gani basi kilichomfanya Kenyatta akatae kabisa Muungano ikiwa ni mwaka mmoja tu tokea atoe tamko la kuwa tayari kushirikiana na Obote na Nyerere? Historia imekuwa shahidi upande wake. Jee, hilo ndilo lililokuwa tukilifanya wakati wote?"

Hayo si maneno yangu. Ni maneno ya Sheikh Aboud Jumbe, aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Alikuwa pia Katibu Mipango wa ASP na baadaye Rais wa ASP. Huyu si HIZBU na sidhani kama anaweza kutuhumiwa kuwa mpinga Mapinduzi au anataka kurudisha Usultani Zanzibar. Hizo ndizo tafakuri zake.

Langu mimi ni moja tu ninalotaka kuongeza. Nalo ni kwamba aina pekee ya Muungano itakayoondoa khofu ya nchi moja kumezwa na nyingine ni ile ambayo kila nchi shiriki itabaki na mamlaka yake kamili kitaifa na kimataifa na kisha kushirikiana kupitia Muungano wa Mkataba (Treaty based Union). Hivyo ndivyo ulivyo Muungano wa Ulaya (European Union) ambao umeendelea kukua na kufikia kuwa na nchi shiriki 27 na ambao mwaka huu umepewa tuzo ya Nobel. Insha'Allah hiyo ndiyo njia ya kufuatwa katika kujenga mahusiano mapya kati ya Tanganyika na Zanzibar yatakayovutia na nchi nyingine kujiunga na kuondoa khofu kama zile za Jomo Kenyatta alizozitoa Agosti 3, 1964.

Friday 21 December 2012

‘Katiba inayoandaliwa ni ya watawala’

JUKWAA la Katiba limesisitiza kuwa Katiba mpya haiwezi kupatikana Aprili 26, 2014 na endapo itafanyika hivyo litazunguka nchi nzima kuhamasisha wananchi kuikataa rasimu ya Katiba hiyo kwa njia ya kura.
Jukwaa hilo limesema litafikia hatua hiyo kwa kuwa Katiba itakayopatikana itakuwa ni ya watawala kwa kuwa wananchi wengi hawajapata fursa ya kutoa maoni yao.
Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa jukwaa hilo, Deus Kibamba, alipozungumza na waandishi wa habari alipokuwa akitoa tathmini ya mchakato wa Katiba kwa mzunguko kwa kwanza.
Alisema endapo nchi inahitaji Katiba ya demokrasia haiwezi kupatikana ndani ya kipindi hicho na kumuonya Mwenyekiti wa Tume ya Katiba, Jaji mstafuu, Joseph Warioba, na wenzake kulitilia maanani suala hilo.
“Dharura imewahi kuligharimu taifa letu na katika nchi nyingine kushindwa kufanya maandalizi kunaweza kusababisha machafuko kwa kutokamilika kwa Katiba mpya huku muafaka ukiwa umeshuka na jamii kutokubaliana kwa mambo mengi ya msingi.”
Pamoja na hayo, jukwaa hilo limetoa hati chafu kwa wakuu wa wilaya wawili, Rosemary Kirigini (Meatu) na Jokiwa Kasunga (Monduli), kwa madai kuwa ni maadui wa mchakato wa Katiba kwa mwaka 2012.
Alisema Kirigini alizuia kumfanyika mkutano wa Katiba ulioandaliwa na asasi ya kiraia ya Mongonet akitaka wasijadili masuala ya Katiba bali mambo mengine wakati Kasunga alizuia mikutano ya uhamasishaji uliokuwa ukifanywa na taasisi ya Pingo’s Forum ambayo ilikuwa na lengo la kuwaelimisha wananchi juu ya mchakato wa Katiba mpya kwa madai ya kutaka taarifa zaidi za taasisi hiyo kabla ya kuruhusu kufaya kazi katika wilaya yake.
“Kutokana na ukubwa wa makosa yaliyofanywa na wakuu hawa wa wilaya na hatari yake katika kufifisha mchakato wa Katiba, Jukwaa la Katiba leo tunatoa hatia maalumu kwa viongozi hawa kama ishara ya kuwatangaza kuwa maadui wa Katiba mpya. Utaratibu huu utaendelea katika muda wote wa uundaji wa Katiba mpya hadi kukamilika,” alisema Kibamba na kuongeza nakala za hati hizo zitapelekwa kwa Rais Jakaya Kikwete.
Alisema kwa mwaka ujao wanatarajiwa kuwapeleka watu wa aina hiyo mahakamani kwa kuwa wanavunja Katiba ibara ya 18.
Akielezea dosari zilizojitokeza katika mzunguko wanne na wa mwisho wa awamu ya kwanza ya ukusanyaji wa maoni ya Katiba ni fursa finyu ya utoaji maoni kwa wananachi.
“Jukwaa la Katiba Tanzania tulishuhudia watu wakijitokeza kwa wingi huku muda uliotengwa ukiendelea kuwa mdogo kwa idadi ya watu wengi waliojitokeza katika mzunguko huu.
“Watazamaji wetu walishuhudia wananchi wakishauriwa kutoa maoni yao kwa njia ya maandishi kwa kuwa wengi wao walikosa fursa ya kuzungumza katika mikutano ya tume,” alisema na kutoa mfano suala hilo limejitokeza eneo la Segerea na Temeke, kata ya Pemba Mnazi.
Alisema suala hilo liliwakatisha tamaa watu wasiojua kusoma na kuandika, ni kinyume na lengo kuwa Katiba itaandikwa na Watanzania wote hata kama hawawezi kusoma wala kuandika.
Aidha alisema wakati mwingine tume ilionekana kuwa na haraka ya kuondoka kutokana na muda waliopangiwa kuwa finyu na walikuwa wakiwahi mikutano mingine.
Alieleza kuwa dosari nyingine waliyoibaini ni kwa vyama kuendelea kuingilia mchakato wa Katiba, jambo linalosababisha kutokea kwa fujo kwa wafuasi kupigana na kutolea mfano vurugu zilizotokea Zanzibar.
Kutokana na hali hiyo, jukwaa hilo limeshauri kuwapo na majadiliano aina ya taifa tunalohitaji kulijenga ikiwa ni pamoja na kukubaliana mipaka ya Katiba tunayoiunda.
“Tujadiliane kwanza tunaunda Katiba ya Muungano? Kama ndiyo tunataka Muungano wa aina gani wa serikali mbili, tatu au wa mkataba,” alisema.
Aidha wanapendekeza mchakato wa Katiba mpya lazima utenganishwe na michakato ya uchaguzi ujao, kwani kuna hatari ya mchakato mmojawapo kuvurugwa.
“Hii itatoa fursa kwa mchakato wa Katiba mpya kuendelea taratibu na bila kuhitaji kukimbizwa hata kama utahitajika kuendelea mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015,” alisema.
Aidha alisema jukwaa hilo litaendelea na kampeni ya kugawa Katiba ya sasa kwa kila Mtanzania na kwamba mpaka sasa kwa kushirikiana na asasi mbalimbali wameshasambaza nakala zaidi ya 300,000 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nakala 10,000 za Katiba ya Zanzibar.
Alisema katika mwaka ujao, jukwaa limejipanga kuendelea na kampeni ya kuongeza nakala za Katiba nukta nundu kwa ajili ya watu wasioona
Chanzo: Tanzania Daima

Thursday 20 December 2012

Kama Chávez ameweza kwa nini wakwetu hawawezi?


Barazani kwa Ahmed Rajab
SIMON Bolivar alikuwa mwanamapinduzi wa Venezuela aliyeiaga dunia Desemba 17, mwaka 1830 akiwa na umri wa miaka 47. Kuna wanaoamini kwamba alikufa kwa kulishwa sumu. Miongoni mwao ni Hugo Chávez, Rais wa Venezuela, ambaye kwa sasa anatibiwa Cuba baada ya kupasuliwa kwa ugonjwa wa saratani.
Oktoba 7, mwaka huu, Chávez kwa mara ya nne alishinda uchaguzi wa urais. Alishinda licha ya ule msaada wa dola zisizopungua milioni 50 ambazo inasemekana Marekani mwaka huu iliwapa wapinzani wake wamshinde.
Lakini yeye ndiye aliyewatwanga na katika uchaguzi wa magavana uliofanywa Jumapili iliyopita chama chake cha Kisoshalisti kiliongeza idadi ya viti vya magavana ilivyoshinda.
Januari, kama atakuwa mzima, Chávez ataapishwa kwa muhula mwingine wa urais wa miaka sita.Chávez anaona fahari kujinasibisha kuwa ni mrithi wa dhati wa Bolivar.Tangu ashike madaraka miaka 13 iliyopita hachoki kukumbusha kwamba siasa zake za ‘Chavismo’ zinalenga kuyatekeleza mapinduzi ya kibolivar.
Vyombo vya habari vya Marekani na vya vibaraka wake vimezoea kumfanyia tashtishi na kumcheza shere Chávez vikimfananisha na bahaluli au Juha Kalulu.Hayo si ya ajabu kwani ni kawaida yao kumkebehi kila kiongozi wa wanyonge anayethubutu kusimama kidete na kwenda kinyume cha ubepari wa utandawazi.
Kwa hakika, Chávez alianza kufanyiwa vitimbwi alipotangaza mara ya mwanzo kwamba atawania urais 1998. Alisema anataka kuijenga upya nchi yake kwa misingi mipya. Wengi walimcheka.
Kwa mtizamo wao katika mwanzo wa karne ya 21 Chávez alikuwa mtu mwenye fikra za kizamani zilizopitwa na wakati. Alikuwa mwanamapinduzi wa mrengo wa kushoto aliyekuwa akiungwa mkono na Wakomunisti wachache waliobaki nchini mwake na makundi kama sita ya mielekeo mbalimbali ya kisoshalisti.
Nadhani Tanzania hii leo akisimama mtu na kusema anataka kuurejesha ujamaa ataonekana mwehu — hata akisema kama ujamaa anaoutaka ni wa aina mpya. Itakuwa hivyo kwa sababu wengi wetu tuna fikra finyu na tumezoea kuyumbishwa na wimbi litokalo nchi za kimagharibi.
Cháveza na mbwembwe za aina yake.Pia ana mtindo wa aina yake wa uongozi ulio na dosari zake lakini wenye kumpa haiba kubwa. Si watu wote wenye kumpenda. Maadui zake wanasema ulimi wake hauna akili. Hauna ubongo.
La muhimu ni kwamba yeye ni miongoni mwa viongozi wachache wa dunia hii wenye kuwajali watu wao. Ni kiongozi ambaye Bara la Afrika halikujaaliwa kumpata. Inasemekana kwamba nchi yake ni ya tano, ikiwa pamoja na Finland, yenye wakaazi wenye furaha mno duniani. Hayo si mafanikio madogo.
Chávez ameweza kuupunguza ufukara kwa hatua mbili muhimu: ya kwanza ni kulitaifisha Shirika la Taifa la Mafuta la Petróleos de Venezuela (PDVSA) na ya pili ni kuugawa kwa haki utajiri wataifa na sio kuwanufaisha wachache tu katika jamii. Umasikini umeporomoka kutoka asilimia 70.8 katika 1996 na sasa ni chini ya asimilia 21.
Ufukara wakutupwa umepungua kutoka asilimia 40 katika 1996 na kufikia sasa kasoro ya asilimia saba. Mwaka 1990 asilimia 7.7 ya watoto walikuwa wakifa kutoka na utapiamlo lakini sasa takwimu hiyo imeshuka na kuwa asilimia 2.9.
Tangu Chávez awe rais idadi ya wasio na ajira imepungua kutoka asilimia 11.3 na kuwa asilimia 7.7. Katika kipindi cha miaka 10 uchumi wa Venezuela umetanuka kwa asilimia 47.7 na leo uchumi huo ni madhubuti kushinda uchumi wa Marekani na nchi kadhaa za Ulaya.
Kuna mafanikio mengine ambayo Venezuela imeyapata ikiongozwa na Chávez. Wazee zaidi ya milioni mbili na laki moja wanalipwa malipo ya uzeeni na idadi hiyo inazidi kuongezeka. Kabla ya Chavez watu 387,000 tu ndio waliokuwa wakilipwa malipo hayo.
Elimu ni bure kutoka ya chekechea hadi ya chuo kikuu. Wananchi milioni tano wanalishwa bure na serikali. Venezuela haina watoto masikini wa mitaani au chokora kama wanavyoitwa Kenya. Dawa zinapatikana kwa bei rahisi. Venezuela pia ina maduka mahsusi yenye kuwauzia watu wa chini vyakula na vitu vingine kwa bei za chini.
Swali la kujiuliza ni: Ilikuwaje Venezuela chini ya Chávez ikaweza kupiga hatua kubwa hivyo katika muda mfupi?
Huenda ukajibu kwamba nchi hiyo inachimba na kusafirisha mafuta na hivyo inajipatia mapato makubwa. Lakini Afrika ya Kusini, Algeria, Angola, Chad, Cameroon, Congo-Brazzaville, Congo-Kinshasa, Cote d’ Ivoire, Equatorial Guinea, Gabon, Ghana, Misri, Morocco, Nigeria, Tunisia, Sudan na Sudan ya Kusini zote hizo zinachimba au zinachimba na kuuza mafuta lakini wengi wa watu wa nchi hizo wanaishi maisha ya dhiki na usumbufu mkubwa.
Alipoingia Ikulu mara ya kwanza 1998, Chávez aliingia akiwa na kikapu cha ahadi akilini mwake. Aliahidi kwamba ataufyeka ufisadi uliokuwa ukiila nchi yake kama unavyoila Tanzania.
Aliahidi kwamba atakuwa na sera mbadala kwa nchi yake, sera ambayo itajitenga kabisa na ile ya uchumi wa kiliberali mamboleo iliyokuwa ikifuatwa nchini humo na ambayo sisi Tanzania na kwingineko Afrika tumeing’ang’ania.
Badala ya kutegemea zile ziitwazo ‘nguvu za soko’ na utandawazi serikali yake ikaanza kupanga maendeleo ya nchi kwa kutumia rasilimali zake na sio kwa kuwategemea wawekezaji. Kadhalika, Chávez alizivunja nguvu Shirika la Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na Benki Kuu ya Dunia katika uendeshaji wa uchumi wa nchi yake.
Alichofanya ni kuthibitisha kwamba kuna sera mbadala za kiuchumi zinazoweza kufuatwa na nchi kama zetu badala ya hizi tunazozikumbatia.
Jengine alilolifanya Chávez ni kuwa macho na kutoipa Marekani nafasi ya kuichezea nchi yake kinyume cha wafanyavyo viongozi wetu. Kwa mfano, amekataa kuziruhusu ndege za Marekani kuingia katika anga ya Venezuela kwa kisingizio cha kuwafukuzia wenye kufanya biashara haramu ya mihadarati. Viongozi wetu wanaipa Marekani fursa hiyo kwa kisingizio cha kuwafukuzia magaidi
Chanzo: raia Mwema

Thursday 13 December 2012

Jinsi Nyerere alivyotawala kimabavu

Barazani kwa Ahmed Rajab
KITU kimoja mataifa ya Magharibi yanachojivunia ni Sheria ya Haki za Binadamu (Bill of Rights). Mataifa hayo na mengine yenye kujigamba kwamba ni ya kidemokrasia halisi yameiingiza sheria hiyo katika katiba zao.
Walimwengu kwa jumla huipigania na kuitetea sheria hiyo kwa sababu wengi wao wanataka tuwe na dunia yenye kuwahakikishia binadamu wote kwamba wataishi maisha ya heshima, ya utu, yenye kuwafanya binadamu wote wawe sawa mbele ya sheria na yenye kuwapa wote uhuru.
Sheria ya Haki za Binadamu ni msingi muhimu wa mfumo wa kidemokrasia na utawala bora. Ndiyo maana tunawaona wanasiasa wengi, walio wema na hata wasio wema, wakiipigia debe sheria hiyo.
Katiba ya sasa ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar zote zinaielezea kwa makini Sheria ya Haki za Binadamu. Katiba zote mbili zilifanyiwa marekebisho mwaka 1984 ili iingizwe hiyo Sheria ya Haki za Binadamu katika kila moja ya katiba hizo.
Wakati wa uhuru mwaka 1961 Tanganyika haikuwa na Sheria ya Haki za Binadamu katika katiba yake. Zanzibar, kwa upande mwingine, iliwahi kuwa na mlango mzima wa Sheria ya Haki za Binadamu katika katiba yake ya uhuru ya mwaka 1963. Katiba hiyo ilifutwa baada ya Mapinduzi ya 1964 na Zanzibar ilipoungana na Tanganyika ikawa inaitumia katiba ya Muungano ambayo kama nilivyogusia haikuwa na Sheria ya Haki za Binadamu.
Tanzania iliiingiza Sheria ya Haki za Binadamu katika katiba yake miaka miwili baada ya viongozi wa nchi za Kiafrika kukutana jijini Nairobi na kuuidhinisha Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu (ACHPR) na pia kuunda Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu yenye makao yake makuu mjini Banjul, Gambia.
Kuna sababu ya kwa nini Tanganyika (na baadaye Tanzania) haikuwa na Sheria ya Haki za Binadamu katika katiba yake. Kwa hakika, Mwalimu Julius Nyerere na wenzake waliokuwa wakipigania uhuru wa Tanganyika hawakutaka kwa makusudi kuliingiza suala hilo katika katiba ya Tanganyika huru.
Kisingizio walichotoa akina Nyerere ni kuwa wakichelea majaji wa kikoloni ambao ndio siku hizo wakisimamia mahakama kwamba huenda wakavitumia vifungu vya Sheria ya Haki za Binadamu ili kuzisambaratisha jitihada za serikali mpya ya wazalendo za kuupatia umma maendeleo ya haraka ya kiuchumi.
Nyerere alikataa katukatu kwamba katiba ya Tanganyika ya wakati wa uhuru iwe na Sheria ya Haki za Binadamu. Alifanya ukaidi huohuo wakati katiba ya Jamhuri ya Tanganyika ilipokuwa inaandaliwa mwaka 1962. Hivyo, katiba zote hizo mbili zilimwezesha Nyerere aitawale nchi kwa mabavu kama walivyofanya wakoloni wa Kiingereza kabla yake.
Taifa jipya la Tanganyika lilifungua macho likijikuta limezirithi sheria za kimabavu. La kusikitisha ni kwamba Nyerere hakufanya jitihada yoyote ya kuzifuta sheria hizo na kuweka sheria zenye kuheshimu haki za binadamu.
Kwa hili Nyerere na Tanganyika hawakuwa peke yao barani Afrika. Nchi nyingi nyingine za Kiafrika zilikuwa na utawala uliojengeka juu ya misingi ya kimabavu na isiyoheshimu haki za binadamu.
Sheria ya Haki za Binadamu iliyoingizwa kwenye Katiba ya Muungano mwaka 1984 ilikuwa isitumike katika mahakama ya kisheria kwa muda wa miaka mitatu ili kuipa Serikali ya Muungano muda wa kutosha wa kuzifuta au kuzibadili sheria zake zote zenye kwenda kinyume na Haki za Binadamu. Hata hivyo, hatua hiyo haikuisaidia Serikali ya Muungano kuzibatilisha sheria zake zote za kimabavu.
Sidhani kama ninakosea nikisema kwamba Tanzania ilikubali kichwa upande kuiingiza Sheria ya Haki za Binadamu katika katiba yake. Nasema hivi kwa sababu ingawa Sheria ya Haki za Binadamu imo ndani ya katiba za Muungano na Zanzibar bado kuna mushkili mkubwa katika utakelezwaji wake. Inavyoonyesha ni kwamba serikali imefanya kusudi iwe ngumu kwa watu binafsi kuzitetea haki zao za kimsingi katika mahakama.
Jingine ni kwamba ingawa katiba zote hizo mbili zinazitambua takriban haki zote za kiraia na za kisiasa hata hivyo kuna nyakati ambapo wananchi wanapata taabu kuzipata au wanazuiwa wasizipate haki zao. Mfano mzuri ni haki ya wananchi ya kuwa na uhuru wa kukusanyika au wa kuandamana wakati wanapotaka. Hizi ni haki za kimsingi za binadamu na uhalali wake si lazima upatikane kwa haki hizo kutajwa ndani ya katiba.
Kwa hali ilivyo Bara na Visiwani haki hizo za kukusanyika na kuandamana zinautegemea sana ukarimu wa Polisi. Wao ndio wenye kutoa kibali cha kufanyika mkutano wa hadhara au maandamano. Wakati wa maandamano Polisi wanatakiwa wawe wanasimamia usalama na amani na si wao kuanza kuichafua amani.
Kesi inayoendelea sasa Zanzibar ya washukiwa wa Uamsho imezidi kufichua jinsi serikali ya huko inavyoikiuka Sheria ya Haki za Binadamu licha ya kuwa imo ndani ya katiba zote mbili, ya Muungano na ya Zanzibar.
Sheria ya Haki za Binadamu inasema kesi ziwe zinaendeshwa kwa haraka. Lakini tukiiangalia hii kesi ya Uamsho tunaona kwamba mahakama yanasotasota katika kuiendesha.
Zaidi ni kwamba washtakiwa ingawa ni watuhumiwa na hawajapatikana na hatia hadi sasa wanatendewa mambo kana kwamba wamekwishapatikana na hatia. Wananyimwa haki zao za kimsingi wakiwa korokoroni na wanafanyiwa mambo ya kuudhalilisha utu wao. Na Bara kuna kesi chungu nzima ambazo kwa miaka mingi baada ya kufunguliwa bado hazijasikilizwa.
Swali la kujiuliza ni: Nani wa kulaumiwa pale wakubwa wa serikali wanapoukiuka huo msingi wa demokrasia halisi? Tumezoea kuwatupia lawama wakubwa wa serikali. Lakini wapo wengine ambao pia wanastahiki kuibeba. Nao ni umma, tukiwemo mimi na wewe.
Umma usiojali serikali inafanya nini au nini haifanyi inachopaswa kufanya ni umma uliopotoka na unaoweza kutiwa shemere na kubururwa kama kondoo na hao wakubwa wa serikali.
Tusitarajie kupewa haki zetu. Lazima wananchi sote tuzipiganie haki zetu zote zikiwa pamoja na zile za kutaka elimu, afya na ajira. Na hatutoweza kufanya hivyo mpaka tujipange. Tuunde jumuiya za kupigania haki zetu, tushurutishe somo la Sheria ya Haki za Binadamu lifundishwe katika maskuli hadi vyuo vikuu. Lengo liwe kuhakikisha kwamba wananchi tusiwe na uwezo wa kusema tu bali pia tuwe na uwezo wa kuamua. Hiyo ndiyo nguvu ya Umma.
Chanzo: Raia Mwema

Tuesday 11 December 2012

Mkutano wa katiba Z’bar vurugu tupu

MIKUTANO ya kukusanya maoni ya upatikanaji wa Katiba Mpya Visiwani Zanzibar, imeingia dosari baada kuzuka ghasia na baadhi ya watu kujeruhiwa kwa kuchomwa visu.

Vurugu hizo ambazo chanzo chake ni siasa, zilitokana na wafuasi wa baadhi ya vyama vya siasa, kuvamia mikutano iliyokuwa ikifanyika Unguja na kusababisha hofu za kiusalama.

Baadhi ya maeneo ambayo wanasiasa hao walivamia mikutano ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kusababisha ivunjike ni Shehia za Magomeni na Mpendae Mkoa wa Mjini Magharibi.Hii ni mara ya kwanza ghasia kuzuka katika mikutano ya kukusanya maoni ya Katiba Mpya visiwani humo.

Tukio la kuchomana visu, lilitokea katika Shehia ya Mpendae baada ya vurugu zilizosababishwa na vijana kuvamia mkutano uliokuwa ufanyike jana mchana.
Vijana hao walianzisha ghasia hizo baada ya kutaka kuvunja utaratibu uliokuwa umewekwa. Walitaka wakae mbele ya wengine waliokuwa wametangulia katika mkutano huo.

Hatua hiyo ilipingwa na kuibua ghasia ziliozababisha watu kadhaa kujeruhiwa kwa visu.

Tukio jingine lililovuruga mkutano huo ni lile lililotokea katika Shehia ya Magomeni, Jumatatu wiki hii baada ya kuibuka kwa mvutano baina ya makundi mawili yenye misimamo tofauti juu ya mfumo wa Muungano; kuna wanaopinga na wanaoukubali.
Misimamo hiyo imeelezwa kujikita katika misingi na sera za vyama vyao vya kisiasa.
Katika misimamo hiyo, CUF kinaamini katika Serikali ya Zanzibar na Tanganyika kila moja kuwa na mamlaka kamili na Muungano uwe wa mkataba wakati, CCM kinasimamia kwenye Serikali mbili; Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Shehia ya Magomeni
Saa mbili kabla mkutano kuanza, watu wengi walifika Uwanja wa Mzalendo ambako mkutano ulitakiwa kufanyika. Walijipanga kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na Tume ambao ni aliyewahi kufika ndiye anayetangulia kutoa maoni.

Hali hiyo ilisababisha wakazi wa Shehia hiyo waliokuwa wenyeji wa mkutano, kukosa nafasi ambayo ingewawezesha kutoa maoni kwa mazungumzo ya ana kwa ana.
Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni, Salmin Awadh Salmin, alisema hawakuwa tayari kuwa wenyeji wa mkutano ambao hawatashiriki akisema waliokuwa wamejipanga wote walifikishwa kituoni hapo kwa magari kwa lengo maalumu la kuwakosesha wenyeji kutoa maoni yao, kwa kuwa inafahamika kuwa wengi wao ni wana CCM.

Hoja hizo alizitoa kwa wajumbe wa Tume ambao pia hawakuridhishwa na hali ya usalama katika eneo hilo kutokana na vurugu zilizokuwa zikifanywa na wafuasi wa CCM na CUF.

“Kwa hali ilivyo, hatuwezi kupata utulivu utakaowezesha tufanye kazi kwa ufanisi na kumaliza mkutano kwa amani bila fujo. Natangaza rasmi kuwa leo hakuna mkutano,” Mwenyekiti wa Timu ya Tume hiyo inayokusanya maoni visiwani hapa, Profesa Mwesiga Baregu.

Akizungumza baada ya kuvunjika kwa mkutano huo, Salmin alisema waliokuwa wamefika kutoa maoni walikuwa wakitaka kunadi misimamo ya vyama vyao akisema hiyo ni hali ya kihistoria inayowakabili wakazi visiwani humo.
“Hata katika kupata huduma za kijamii, siasa inapewa kupaumbele na hili ndilo chimbuko la matatizo yote haya, ndiyo maana hata maoni yanayotolewa ni ya aina mbili, Muungano udumu au uwe wa mkataba na serikali mbili.

Dalili za vurugu
Dalili za kuwapo kwa vurugu zilianzia kwenye mkutano uliofanyika Jumatatu asubuhi kwenye Viwanja vya Kibanda Maiti katika Shehiya ya Kwa-Alamsha, ambako watu waliotaka Muungano ubaki, walizomewa huku waliotaka Serikali ya Zanzibar na Tanganyika kila moja ikiwa na mamlaka kamili, muungano uwe wa mkataba walishangiliwa.

Hali hiyo ilitawala mkutano huo bila kujali jitihada za Profesa Baregu kukemea mara kwa mara hali hiyo. Pamoja na kwamba maoni yatafanyiwa mchujo, Wananchi hao wanaamini kuwa upande utakaotoa maoni kwa wingi ndiyo utakaoshinda kwa matakwa yao kuingizwa kwenye Katiba Mpya.

Mbunge amshambulia Mratibu
Katika mkutano uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Wandarasi, Shehia ya Meya, Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Faharia Shomari alimshambulia Mratibu wa shughuli za Tume visiwani humo, Ahmed Haji Saadat kwa maneno akiwambia:
“Mimi ni Mjumbe wa Tume ya Bunge ya Sheria na Katiba. Nilihusika kutunga sheria inayowaongoza kufanya kazi hii, inatakiwa wakazi wa shehia mnayofanyia mkutano watoe maoni kwa kuzungumza, wengine wapewe fomu; tatizo wewe unajidai mkubwa kuliko hata tume yenyewe. Mikutano yote umeivuruga wewe, tangu mwanzo nilikwambia, kiko wapi sasa,” alisema mbunge kwa hasira.

baada ya mashambulizi hayo, Saadat naye alijibu: “Mheshimiwa, ninakuheshimu sana, ikiwa tatizo unaliona ndani ya sheria na unakiri ulihusika kutunga sheria hiyo bila kueleza uzoefu ulionao kwa mazingira ya Zanzibar, wewe ni sehemu ya tatizo. Tangu nilipokuwa Mji Mkongwe umekuwa ukinifuata kwa maneno, tatizo lako hasa nini?”
Zogo hilo lilikuwa kubwa na kusababisha askari kumwondoa mbunge huyo kumpeleka pembeni. Lakini baada ya muda, mbunge huyo alijivuta mpaka alikokuwa Saadat na kuanza tena kumwandama kwa maneno akisema: “Kiko wapi? Jana hamkufanya mkutano kwa kujidai kwako, leo pia zogo hilo, huenda msiufanye kwa kujidai mkubwa lol, unajidai una nguvu kuliko hata wajumbe wa tume? Kiko wapi sasa?”
Maneno hayo yalimkera Mratibu huyo ambaye alimtaka athibitishe anayomtuhumu kwa maandishi.

Iliwalazimu askari polisi kuingilia kati tena kati na kumshauri Saadati kumfungulia mashtaka mbunge huyo.

Mbunge huyo alitoa maoni yake kwenye Jimbo la Mji Mkongwe, Vuga na kuhudhuria mkutano wa maoni uliyofanyika siku hiyo hiyo kwenye Hoteli ya Bwawani ambako inadaiwa kuwa ndiko alikoanza kuzozana na Saadat; akimtuhumu kupendelea wanaotaka muungano uwe wa mkataba na Serikali ya Zanzibar yenye mamlaka yake kamili.

Tuhuma hizo zilitokana na Saadat kukataa kuruhusu kundi la wanawake ambao Shomari alitaka wakatoe maoni tofauti na utaratibu uliowekwa ambao unampa nafasi aliyewahi kufika na kujipanga kwenye foleni kutoa maoni kwanza.

“Nimeishakuona unapendelea watu wa mkataba, subiri nitakuripoti kwa (mmoja wa wajumbe ambaye pia ni kada wa CCM),” Shomari alisikika akimweleza Saadat ambaye alimjibu kuwa kinachoangaliwa si nani wala itikadi gani, bali utaratibu uliowekwa tu
Chanzo: Mwananchi

Sunday 9 December 2012

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni sawa na ndoa ya mkeka’

MCHAKATO wa utoaji wa maoni ya Katiba Mpya unaendelea kwenye mikoa sita katika awamu hii ya nne. Mikoa ambayo Tume iko katika kuchukua maoni ya wananchi ni Arusha, Dar es Salaam, Mara, Simiyu, Geita pamoja na Zanzibar Mjini Magharibi. Katika mikutano hiyo ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, wananchi wamekuwa wakitoa maoni mengi yenye hoja tofauti.
Katika mikutano hiyo, wajumbe wa Tume wamekuwa wakiwahimiza wananchi kushiriki kwa uhuru katika kutoa maoni yao bila hofu. Wito huo wa Tume umekuwa ni jambo la msingi ikizingatiwa kwamba Watanzania wengi wamekuwa na tabia ya kuogopa na hata kukosa ujasiri wa kuzungumza hadharani kwa kuikosoa ama Serikali au viongozi wake kwa hofu ya kuogopa kukamatwa au kufuatiliwa na vyombo vya usalama.
Katika mchakato unaoendelea wa ukusanyaji wa maoni ya wananchi, imeshuhudiwa wananchi hao wakijieleza kwa uhuru bila hofu kwenye mikutano mbalimbali ya Tume.
Hii ni haki yao ya kikatiba kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kitu ambacho wananchi kwenye kila mkutano wa Tume wamekizungumzia ni suala la Muungano wa Serikali tatu.
Wananchi wengi wamekuwa wakisisitiza kuwa Katiba Mpya haina budi kuitambua na kuirejesha Serikali ya Tanganyika. Wananchi hao wamesema kuwa Serikali ya Tanganyika ni haki ya Watanganyika kama ilivyo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
“Watanganyika tumekosa fursa ya kuwa na Serikali tofauti na wenzetu Wazinzibari ambao wao wanayo Serikali. Kwa hiyo nataka kuona kuwa Katiba Mpya inairejesha Serikali ya Tanganyika ili kuleta uwiano sawa kati ya pande mbili za Muungano,” anasema Haji Juma mkazi wa Kata ya Jangwani Jijini Dar es Salaam.
Hoja hiyo inaungwa mkono na Thadeus Mangia mkazi wa Tabata Kimanga ambaye ameufananisha muundo wa Muungano uliopo kuwa sawa na ndoa ya mkeka. Anasema kuwa Katiba Mpya inapaswa kuheshimu uamuzi wa wananchi juu ya aina gani ya Muungano wanaoutaka na siyo kulazimishwa waishi kwenye Muungano wasioutaka. Mangia anasema kuwa muundo unaowafaa Watanzania kwa sasa ni Muungano wa Serikali tatu.
Mangia anasema kuwa Muungano wa Serikali tatu utaondoa manung’uniko yaliyopo miongoni mwa wananchi kuwa upande fulani unaonewa na upande fulani wa Muungano ndiyo unaofaidika.
Anasema suluhu ya matatizo ya Muungano ni kuirejesha Serikali ya Tanganyika kama ilivyo kwa Serikali ya Zanzibar kisha iundwe Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Wananchi hao wanasisitiza kuwa katika Muungano huo walioathirika ni Watanganyika kwa kupoteza Serikali yao. Wanasema Wazanzibari wana Rais na Serikali tangu mwanzo wa Muungano, lakini Watanganyika wamepoteza vyote, yaani Rais na Serikali. Kutokana na hali hiyo, Mwalimu Florah Ishengoma (50) kutoka Tabata Kimanga anasema kuwa Muungano uwe wa Serikali moja na hilo likishindikana basi Serikali ziwe tatu ili na Watanganyika nao wapate haki yao.
“Kila siku wenzetu Wazanzibari wanalalamika kuwa wao wamemezwa na muundo wa Muungano huu. Sasa ili kuondoa malalamiko, napendekeza kuwapo Serikali tatu, yaani ya Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Kama hilo haliwezekani napendekeza tuwe na Serikali moja, Rais mmoja na mawaziri wakuu wawili, mmoja wa Zanzibar na mwingine wa Tanganyika, na hao mawaziri wakuu wachaguliwe na Bunge,” anasema Hamad Tao mkazi wa Kata ya Ilala.
Wananchi hao wamezidi kusisitiza kuwa Katiba iliyopo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inapotosha historia kuhusu suala la Muungano kwa kuwa imeiua Tanganyika na badala yake imeanzisha kitu kinachoitwa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani. Wanasema kuwa hakuna nchi inayoitwa Tanzania Bara iliyoungana na Tanzania Visiwani ikatokea Tanzania.
“Hakujawahi kuwepo kwa nchi inayoitwa Tanzania Bara wala Tanzania Visiwani. Haya ni mapungufu ambayo Katiba Mpya inatakiwa kuyarekebisha ili historia ibaki kama ilivyokuwa. Tanganyika itambulike kwa kuwa Muungano uliopo ni kati ya nchi ya Tanganyika na nchi ya Zanzibar,” anasema Adventina Ndibalema mkazi wa Kimara Korogwe.
Katika Sura ya Kwanza, Ibara ya (1) na Ibara ya 2(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 zinaeleza maana ya Muungano. Ibara hizo kwa pamoja zinasema kuwa Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano. Inaendelea kufafanua kuwa eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.
Ibara hizi hazisemi chochote kuhusu nchi za Tanganyika na Zanzibar, bali zimebadilishwa jina na kuitwa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.
Hapa ndipo wananchi wengi kwenye mikutano ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba wanapotaka Serikali ya Tanganyika irejeshwe kama ilivyokuwa kwa Serikali ya Zanzibar ambayo ipo tangu Muungano uanzishwe, Aprili 26, 1964.
Mwenyekiti wa Chama cha NLD (National League for Democracy) Dk Emmanuel Makaidi ameiambia Tume kuwa Serikali ya Tanganyika iliyouawa wakati wa Muungano inatakiwa kurejeshwa kupitia Katiba ijayo. Dk Makaidi anasema kuwa Wazanzibari katika Katiba yao, wanaitambua nchi yao, lakini Tanganyika haitambuliki mahali popote.
Kutokana na sintofahamu iliyopo kuhusu Tanganyika, Dk Makaidi kama ilivyo kwa wananchi wengine anaona kuwa Serikali ya Tanganyika ni haki ya Watanganyika ambayo hainabudi kurejeshwa kupitia mchakato huu wa kurekebisha Katiba ya nchi. Anasema kuwa kuuawa kwa Serikali ya Tanganyika ni kesi ambayo kwa muda mrefu haikupata majibu, lakini sasa majibu yake yapatikane kupitia Katiba ijayo.
“Haiwezekani tuwe kwenye Muungano ambao unaruhusu upande mmoja wa Muungano kuwa na Serikali yake, Bunge lake na kila kitu, halafu upande mwingine uwe umepoteza Serikali na mambo yake yote. Wenzetu wa Zanzibar wanayo Serikali lakini Tanganyika haijulikani iko wapi, ni bora tuungane na Burundi kuliko kuendelea kuwa kwenye Muungano huu,” anasema Abeid Rutozi ambaye kitaaluma ni mkalimani kutoka Kata ya Saranga jijini Dar es Salaam.

Chanzo: Mwananchi

Ukweli kuhusu Uhuru wa Tanzania

SHEREHE ZA UHURU ‘FEKI’ WA TANZANIA…!
• Msimu wa Tanganyika kuizuga dunia wawadia!
• Hufanya sherehe za mamilioni ya walipa kodi dunia nzima!
Tarehe 09 Disemba mwaka huu, yatajwa kitaifa na kimataifa kuwa ndio siku ya Uhuru wa Tanzania ambao hadi siku hio, Taifa hilo la ‘kufikirika’ la Riwaya za Shaaban Robert litatimiza miaka 51, tangu lipate uhuru kutoka kwa Wakoloni wa nchi jirani ya ‘Kusadikika’ pia ya Shaaban Robert.
Kwa wasiokuwa wasomaji wa Riwaya za Mwandishi mahiri, na baba wa fasihi ya Kiswahili hayati Shaabani Bin Ufukwe (Shaaban Robert), nataka niwakumbushe tu kuwa katika Riwaya zake mbili za Kusadikika na Kufikirika, alijaribu kusawili mazingira ya nchi zisizokuwepo kiuhalisia bali kivitendo na muonekano wa kitaswira nchi hizo hufanywa zionekane zipo au huwepo kimawazo. Lakini kiuhakiki nchi hizo zaweza kuwa sawa na nchi yoyote ile yenye sifa zilizotajwa na mwandishi huyo.
Nalazimika kujenga hoja kuwa uhuru wa Tanzania ni wa nchi za Kusadikika na kufikirika kwa sababu dhana nzima ya uhuru na nchi yenyewe haipo kiuhalisia na kimantiki. Kwanza hakuna nchi ambayo inaitwa Tanzania kiukweli hasa na kama ni jina tu, ‘Tanzania’ ni sawa na jina lilibuniwa na watu la Dar es Salaam kuiita ‘Bongo’ na si vyenginevyo. Pili, hata kama nchi hiyo tunalazimishwa kuamini kuwa ipo, basi haihusiani kabisa na dhana ya uhuru na Ukombozi wan chi za Afrika na ndio hata ukifuatilia harakati za uhuru na ukombozi wa bara la Afrika utakutia nchi iitwayo Tanzania haimo kabisa.
Dhana ya uhuru wa nchi haihitaji mtu aliesoma sana kuijua fasili yake. Kwani kimsingi Uhuru ni hatua ya nchi kujipatia nafasi ya kujitawala yenyewe na uwezo wa kujifanyia maamuzi ambapo kabla ilikuwa mamlaka hayo hayakuwa mikononi mwa Wazalendo au wananchi wenyewe, bali yalikuwa chini ya mikono ya wageni waitwao Wakoloni.
Kwa mantiki hii tunarudia kusema kuwa, Tanzania haikuwepo kabla na hata muda mfupi baada ya Uhuru wa bara na Visiwani, itakuwaje iwe nchi huru? Unaposema Uhuru wa Tanzania, kwa wenye akili za kidadisi watakuuliza nchi hio ilitawaliwa na nani? Labda tujikumbushe historia kidogo ya Afrika Mashariki. Zanzibar ilitawaliwa na Muarabu, Kenya Muingereza, Uganda Muingereza, na Tanganyika au German East Africa, ilitawaliwa na Mjerumani.
Hili ni somo la Hitoria ya darasa la sita na la saba hapa kwetu.
Pia tujikumbushe tarehe muhimu za Uhuru wa nchi hizo. Kenya ilipata Uhuru tarehe 10 Disemba 1963, Uganda tarehe 09 Oktoba 1962, Zanzibar 12 Disemba, 1963, na Tanganyika Tarehe 09 Disemba, 1961. Kwa hivyo, hapa hapana cha kuwazuga watu, kwani kwa hakika katika nchi hizi kuu nne za Afrika Mashariki utaona kuwa Tanzania haimo.
Juu ya hayo, hivi sasa kuna mabango kila pahala duniani na katika mitandao ya jamii inayosema na kunadi Sherehe za kufa mtu za Uhuru wa Tanzania kutimiza miaka 51. Wenzetu wa bara wamezoea kuwazuga Wazanzibari kwa sababu ndio ‘mazuzu’ labda au ‘mayakhe’ au ‘mdebwedo’ kama walivyozoea kutuita, na wanafikiria kuwa Wazanzibari waliokuwa ‘mazuzu’ wakati huo watakuwa mazuzu na vizazi vyao vijavyo kiasi ya kutoweza kujua hata hesabu ya kutoa na kujumlisha.
Kwa vile wanaaamini waliweza kuitawala Zanzibar kwa hadaa, ujanja, na kuwazuga wazanzibari kwa kuwapa vyeo na kuwatisha wengine kwa adhabu na mambo mbali mbali, wenzetu hawa bado wanaamini kuwa dunia nzima ina mazuzu kama hivi wanvyowaona Wazanzibari walioshindwa kujuwa hesabu ya Mwalimu ya 1+ 1 = 2 ( Wazanzibari walisema 1+1=3).
Baada ya kuona kuwa hatujui hesabu ndio hapo ukaona kuwa Uhuru wa Tanganyika unatimiza miaka 51 yaani ni sawa na 2012-1961, wao wakidhani na hesabu hii itaushinda pia.Cha kushangaza, hesabu ya darasa la kwanza hadi la tatu tu hii na bado dunia nzima inazugwa ik iamini kuwa Tanzania leo inatimiza miaka 51 ya uhuru wakati nchi yenyewe hata haipo, imeundwa tu kutokana na Riwaya za Shaaban Robert za kusadikika na kufikirika.
Mpaka hapa naamini umeweza kuona kuwa wenzetu wa bara wanatumia hila na mbinu kuudanganya Ulimwengu na huku wakitumia pesa zisikuwa kidogo za walipa kodi ndani na nje ya nchi kwa kusherehekea Uhuru wa nchi isiyokuwepo katika nchi zilizotawaliwa. Huu ni upotoshaji mkubwa wa dunia na kusema kweli unaiondolea hadhi nchi yetu kwa kusema Uongo ulio dhahiri mbele ya kadamnasi ya kimataifa.
Leo hii kuna Sherehe kila pahali: London, Canada, Italia, China, Ufaransa, Ujerumani, Marekani na nchi zote; eti ‘Miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania’. Hii haileti maana wala haina mvuto wowote zaidi ya kuuonesha Umma ufinyu wetu wa mawazo na fikira za kutojua maana ya neno Uhuru na baya zaidi hata kutojua historia yetu na hesabu ya kujumlisha na kutoa tu ambayo kila mtoto wetu wa darasa la kwanza na la pili anaijua.
Nionavyo, Ipo haja tubadilike. Hakuna ubaya kusema ukweli hata kama unauma. Wala haitaibabua sura haiba ya bara kwa kuandika na kujitangazia ‘Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika’. Si vibaya kwani huu ndio ukweli. Ni afadhali tuseme ukweli tuepuke kuchekwa na kuadhirishwa.
Nakumbuka mwaka jana pale London, kuna Mzanzibari mmoja alifanikiwa kupenya na kuingia katika Sherehe za Miaka 50 ya uhuru wa ‘Tanzania’. Alipofika alimuuliza balozi ‘Hivi Tanzania ilipata uhuru kutoka kwa nani?’. Balozi hakuwa na Jibu. Baada ya hili, tulifikiri watajirekebisha, lakini ndio kwanza wanazidi kujitangaza hivyo ilhali dunia inajuwa kuwa huu wanaoufanya ni Uongo wa mchana, kuzimu hakuna nyota.
Kwa muungwana ni wajibu ukweli usemwe, hakuna uhuru wa Tanzania. Tusidanganyane na kudanganya watu kwani mwisho tutashindwa kwani ukisema uongo, Ukweli haujifichi,na ukiibuka ukweli kinachofata ni kuona aibu tu. Kwani wazungu husema ‘Unaweza kuwadanganya baadhi ya watu, baadhi wa wakati, lakini huwezi kuwadanganya watu wote, siku zote’.

Thursday 29 November 2012

Karume “mpuuzi”, lakini ukweli wake mchungu

MAKALA hii itahitimisha tathmini yangu kuhusu Mkutano Mkuu wa 8 wa CCM uliofanyika Dodoma tangu Novemba 11 hadi Novemba 14 mwaka huu.
Kwa kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama dola, vimbwanga vyake huwa vinachanganya watu na kuamini kuwa kila baada ya Mkutano Mkuu, CCM huwa inazaliwa upya.
Imani hii imejengeka kutokana na ukweli kuwa, kabla ya Mkutano Mkuu, huwa kuna dalili za migawanyiko na mipango kadhaa ya makundi kutaka agenda zao zishinde.
Kutokana na udhibiti wa vyombo vya dola pamoja na ushabiki uliopitiliza, mipango hiyo huwa inakwama na kuwafanya watu wengi kuamini kuwa CCM ina wenyewe, na wenyewe hao huwa wanaifanya izaliwe upya kila baada ya Mkutano Mkuu!
Historia ya dhana hii ni ndefu, na wahanga (victims) wa mkakati huu kwa miaka ya karibuni ni Salmin Amour (Komandoo), Mzee John Malecela, Dk. Gharib Bilal, Samuel Sitta na sasa Edward Lowassa.
Kwa miaka ya nyuma wanakumbukwa Mzee Aboud Jumbe na Sharrif Hamad. Kwa sababu zilizo wazi, mkakati huu wa kuipa uhai mpya CCM huwa unawaathiri sana Wazanzibari kuliko Watanganyika.
Rais Karume na “upuuzi” wake
Kama Makamu Mwenyekiti anayemaliza muda wake, rais mstaafu Amani Karume alikaribishwa kutoa nasaha zake siku ya kufunga mkutano. Alitoa hotuba, ambayo hivi sasa inaitwa ya kipuuzi huko Magogoni na mtaa wa Lumumba.
Hakuna aliyetarajia kuwa Karume angesema maneno aliyoyasema siku hiyo kiasi cha Mwenyekiti Jakaya Kikwete kukiri kuwa “hajawahi kumwona amefurahi kiasi hicho” kama alivyomwona siku hiyo.
Mara kadhaa hotuba yake ilikatishwa na watu waliomzomea na kumtaka amalize na kukaa. Hii ikakumbusha enzi za uenyekiti wa Benjamin Mkapa wakati wanamtandao wa Kikwete walipokuwa wakimzomea kila mtu aliyetaka kuhoji matumizi ya rushwa katika mkutano huo.
Mzee Joseph Butiku anaikumbuka hii na aliiandikia barua rasmi kwa Mwenyekiti Mkapa. Hii itukumbushe kuwa zomea zomea haikuanza na CHADEMA katika mikutano.
Alipozomewa sana, Rais Karume akawafananisha wazomeaji na vinywa vya samaki! Wapo waliodai, Rais Karume alikuwa kalewa sana konyagi siku hiyo. Awe alilewa au hakulewa; ni mpuuzi au si mpuuzi; kwangu mimi si habari. Habari muhimu ni yale aliyoyasema kwa dakika alizopewa.
Karume alizungumzia kadi yake ya ASP (Afro Shiraz Party); akaelezea madhumuni ya ASP; akamwuliza Dk. Shein ikiwa yeye anayo kadi yake ya ASP. Moja ya madhumuni ya ASP akakumbusha kuwa ni kulinda uhuru wa Zanzibar na watu wake. Ndipo akahoji wale wanaowazuia wenzao wasitoe maoni yao kuhusu Muungano.
Akamkumbusha Rais Kikwete kuwa alitoa ruhusa kila mtu aseme anachotaka wakati wa mchakato wa kutoa maoni ya katiba mpya. Akahoji iweje sasa wengine wanakamatwa kwa kutoa maoni yao. Karume akakumbusha jinsi CCM ilivyopoteza baadhi ya majimbo kwa sababu ya kupuuzia maoni ya wananchi. Akakumbusha suala la zamu kati ya mbunge na mwakilishi katika jimbo fulani. Wazomeaji hawakutaka kusikia haya wakamwimbia taarabu ya “uamsho uamsho”.
Niseme wazi hata kama nilichoka nikakaa nje ya ukumbi wakati anaongea, Karume alisema mambo ya maana kuliko hotuba za masaa zilizotolewa na waheshimiwa wengine. Kwa muda mfupi, Karume aliuzodoa udikteta unaoabudiwa ndani ya CCM; alibainisha hatari zinazoukabili Muungano; alikumbusha habari za zamu za kuongoza nchi hii iliyotokana na nchi mbili; na zaidi sana alisema kutoka moyoni kuwa ASP haijafa kwa sababu waliokuwa wanachama wake wangali bado hai. CCM tumeze au tuteme, huo ndio ukweli kutoka kwa Karume, ambao sasa unaitwa ni upuuzi na akina Nape Nnauye.
Kulialia na kulalama kulizidi mno
Kwa siku tatu, Watanzania walishuhudia wajumbe zaidi ya 2000 wakilialia na kulalamika ndani ya ukumbi. Mwenyekiti alizindua uliaji huo na kupokewa na wajumbe kwenye vikao visivyo rasmi katika nyumba za kulala wageni na kwenye magari. Kivuli cha Chama cha Denokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kiliwatesa sana wajumbe na kuwafanya viongozi kupoteza mwelekeo na kuanza kutukana ovyo ovyo.
Haikutarajiwa kuwa Mwenyekiti naye angeingia katika mtego huo, pale alipojikuta anawatukana wapinzani na hasa CHADEMA kwa kuwaita “watu wazima ovyo”, au pale ndani ya NEC alipojikuta anatumia muda mwingi kumpamba Nape Nnauye kwa kuwa anajua kutukanana na CHADEMA. Hata pale alipokumbushwa na rafiki yake kuwa kuitukana CHADEMA si lazima kuijenge CCM, yeye aliishia kusema “wamezidi acha Nape awashughulikie”. Kazi inayomshinda yeye, anaona ni bora aifanye Nape. Kama Mzee Rashidi Kawawa alivyokuwa kwa Mwalimu, Nape ndivyo kwa Kikwete!
Mzee mkorofi kutoka Nyanda za Kusini alihoji, inakuwaje CHADEMA iwe tishio kwa CCM kuliko ufisadi na rushwa ulivyo tishio? CHADEMA inakuwaje tishio kuliko “unduguneizesheni” unaotafutiwa nafasi ya kutambuliwa kwenye katiba ya chama chetu?
Akasema, inakuwaje washauri wakuu wa Mwenyekiti wa chama chetu kuhusu masuala ya chama, si vikao bali ni wanausalama waliojaa fitina? Huyu naye alikuwa analalama sawa tu na wengi waliokuwa wanalalamika kwa siku tatu za mkutano.
Membe: Alimzamisha Mangula; Amemuibua tena.
Nafasi ya Bernard Membe kwa siasa za taifa hili kwa siku za usoni ilikuwa katika mtihani mgumu sana. Kambi ya rafiki yake wa zamani Edward Lowassa ilipania kumzamisha lakini akaokolewa na Kikwete na familia yake.
Kikwete alimsaidia kwa kubadili ratiba za upigaji kura, wakati familia yake (mkewe na mtoto wake) walihaha kila kona kumtafutia kura Bernard Membe. Taifa hili siku moja litadai kujua ukweli wa uhasama na urafiki wa watu hawa watatu – Membe, Kikwete na Lowassa. Jina Kikwete limekaa katikati kwa makusudi. Yeye ni ufunguo wa kitendawili hiki. Hili tuliache kwa sasa.
Mzee Philip Mangula, akaibuka ghafla kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara. Ni huyu huyu ambaye kundi la mtandao lililomwingiza Ikulu Kikwete lilidai alilitesa sana wakati wa kampeini na kuamua kumtosa mara baada ya Kikwete kuapishwa.
Yasemekana, Benard Membe, kachero mzoefu na kiini cha mikakati ya wana mtandao asilia, alimwambia Kikwete kuwa Mangula aliwapa taabu sana hivyo aondolewe kwenye nafasi ya ukatibu mkuu wa chama. Haikuishia hapo, Mzee Mangula alipojaribu kuibukia Iringa kama Mwenyekiti wa Mkoa alishughulikiwa vikali na kuangushwa na mtu asiyefanana na CCM kwa vigezo vyote.
Mzee Mangula alikiri baadaye kuwa ndani ya CCM uongozi uko mnadani na wapiga kura hawataki tena vipeperushi vya wagombea, bali wanataka “vipeperushwa”. Mzee Mangula, kila anapokumbushwa harakati za wana mtandao, huwa anatania kuwa yeye aliponzwa na “faili maalumu”.
Kuna habari kuwa Mzee Mangula kaibuka kwa mkono wa Membe. Kwamba, vikao kadhaa vilifanyika Makambako kati ya wawili hawa. Iwe kwa Membe kujituma au kutumwa, ni kwamba walikutana na agenda ilikuwa ni uchaguzi katika Mkutano Mkuu wa 8.
Aliombwa radhi au hakuombwa, hilo sasa si habari. Habari ni kuwa, Mkutano Mkuu umempitisha Mzee Mangula kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM lakini mshenga mkuu alikuwa Membe. Kama ushenga huu ulikuwa ni kwa manufaa ya chama au kwa manufaa ya mtandao wake anaouunda kwa ajili ya 2015, ni suala la wakati.
Ikiwa ni kweli, basi itakuwa vigumu kukemea mitandao ndani ya chama hiki kikongwe. Kama mtandao wa Membe ni halali, wa Lowassa hauwezi kuwa haramu. Kama Kikwete aliingia kwa mtandao, ni vigumu kuifikiria CCM na urais bila mtandao. Na tumejifunza kwa uchungu kuwa mtandao hauishii katika uchaguzi kwa sababu, baada ya mtu wao kuchaguliwa, kinachofuata ni kufaidi jasho na matunda ya kazi.
Kwa walioshindwa, kuna kazi ya kutathmini ni wapi wamekwama na kuazimia aluta continua. Ni ndoto kuambiana kuvunja makundi wakati anayeshinda na kuingia Ikulu anaendelea na kundi lake.
Jambo moja tu Mzee Mangula alizingatie. Membe anayedaiwa kumzamisha baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 mbele ya Kikwete, hawezi kugeuka leo na kumtetea kuwa ni mtu mzuri anayekifaa chama. Kwa nini hakufaa mwaka 2005 chini ya Mwenyekiti huyuhuyu? Membe ni yule yule, Mwenyekiti ni yule yule, chama ni kile kile na Mangula ni yule yule! Ni kitu gani kimebadilika kumfanya Mangula asiyefaa mwaka 2005, afae mwaka 2012?
Kinachoonekana lakini hakizumguziwi waziwazi, ni ukweli kuwa Kikwete na Membe wanamwona swahiba/hasimu wao Lowassa kuwa sasa ni zaidi ya mgombea urais wa CCM 2015. Kwao, Lowassa amegeuka kuwa chama; ameiteka CCM mbele ya macho yao na wanadhani Mangula atawasaidia kuiokomboa CCM iliyo mateka mikononi mwa Lowassa. Kikwete na Membe hawajiulizi ni kitu gani kimemjenga Lowassa na kumfanya kuiteka CCM.
Kitendo cha kumkimbilia aliyekuwa “adui” yao na chama chao kuwa aje kuwasaidia kukijenga chama walichokibomoa kwa mikono yao, hakieleweki. Wengi tulidhani, Mkutano Mkuu ungepata nafasi ya kutathmini hali hii, badala yake tukaambulia kulialia na vijembe visivyo na mpangilio. Tusubiri Mkutano Mkuu mwingine maalumu au ule wa 2017.
Chanzo: Raia Mwema

Tuesday 27 November 2012

Siasa isiingilie uhuru wa Mahakama Z’bar

Na Salim Said Salim
TUNAAMBIWA kuwa hapa nyumbani na nje katika mfumo wa utawala bora wa haki na sheria dhamana kwa mshitakiwa ni haki, japokuwa mahakama ndiyo yenye uamuzi wa mwisho juu ya suala hili.
Nchi nyingi zenye utawala wa demokrasia zimeweka utaratibu unaojaribu kwa kiasi fulani kuhakikisha mahakama hazitumii vibaya mamlaka yake katika suala la dhamana.
Hii ni kwa sababu ipo dhana yenye nguvu inayosema kumuwekea mshitakiwa masharti magumu ya dhamana yanatoa tafsiri ya kuwa sawa na kumnyima dhamana au kuanza kumuadhibu mtuhata kabla hajatiwa hatiani.
Katika baadhi ya kesi zinazoendelea Zanzibar hivi, hasa zile zenye harufu ya kisiasa, kuchimba almasi au dhahabu ni rahisi kuliko kupata dhamana.
Hali hii imesababisha baadhi ya watu,Visiwani na nje, kuuliza kwa kiasi gani mahakama za Zanzibar zipo huru?
Mimi ukiniuliza jibu langu ni kwamba nasikia kuwa zipo huru, lakini sizioni kuwa huru.
Baadhi ya watu Visiwani, hasa wanasheria, wanasema panapokuwepo kesi zenye mashiko ya kisiasa ya aina moja au nyingine mahakama za Zanzibar huwa zinendeshwa kwa kitufe cha mbali (remote control).
Maelezo haya yamepata nguvu kutokana na mahakimu na majaji kueleza mara nyingi kuwa wamekuwa wakipewa amri na wakubwa, baadhi ya wakati kwa kutumiwa vikaratasi, juu ya namna wanavyotakiwa kuendesha kesi.
Unapokuwa na mtindo wa aina hii, hata ikiwa kwa kesi chache sana, basi majumuisho unayopata ni kuwa mahakama hazipo huru na kwamba zimegeuzwa kuwa sehemu ya utawala badala ya kuwa eneo lililo huru na linalotoa na kulinda haki.
Mahakama za Zanzibar hivi sasa zimekuwa zikitoa masharti ya dhamana ambayo unaweza kusema magumu sana au hayatekelezeki na hali hii imezusha wasi wasi juu ya huo uhuru wa mahakama unazungumzwa.
Zanzibar imekuwa na sifa ya kuweka masharti magumu ya mtuhumiwa kupewa dhamana na baadhi ya masharti haya ni ya aina yake na ya kipekee ambayo husikii kuwekwa Tanzania Bara au katika nchi yoyote ile inayojinadi kuwa na mazingira ya utawala wa haki na sheria.
Baadhi ya masharti haya, kama nilivyoeleza siku za nyuma, yana sura chafu ya kuwabagua raia na kuwaweka katika madaraja mawili, moja la watukufu na lingine ni la watu ambao mahakama haitaki kuwaamini. Hawa watukufu ni wale wanaofanya kazi serikalini na wasiostahiki kuaminiwa na kuheshimiwa ni wale ambao sio wafanyakazi wa serikali.
Siku hizi imekuwa kawaida kusikia mshitakiwa anaambiwa kwamba wadhamini wake lazima wawe watumishi wa serikali wakati inajulikana wazi kuwa mtumishi wa serikali hawezi kuhatarisha ajira yake kwa kukubali kuwa mdhamini katika kesi ambayo watuhumiwa wake wamekuwa wakizungumzwa na viongozi wakuu wa nchi.
Mfano mmoja ni wa kesi inayowakabili viongozi wa jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho. Hivi mfanyakazi gani wa serikali atajitokeza kuwawekea dhamana?
Tusidanganyane, huu sio mchezo mzuri na ndio maana wananchi wengi na hata hao tunaowaita washirika wetu wa maendeleo wanauona hauonyeshi haki kutendeka.
Au vipi kijana ambaye hana hata kiwanja utamtaka aweke dhamana waraka wa nyumba wakati hata hivyo viwanja hugawiana wakubwa na watu wanaohusika na ugawaji hujigawia wao, watoto, wake zao na hata wajukuu? (angalia ripoti ya tume ya uchunguzi juu ya ugawaji wa viwanja).
Kama majina ya kweli na sio ya bandia ya watu waliopewa viwanja yatawekwa hadharani utaona watu hoe hae kama akina Salim Said Salim ambao hawapo tayari kuwaabudu viongozi kwa ajili ya kutaka vyeo au kulinda urafiki hutayaona.
Majina ya waliopewa viwanja yatawekwa hadharani. Sasa vipi mtu masikini utamtaka aweke kaburi la mzee wake.
Jamani zama za kuifanya Zanzibar kuwa na haki ya kufanya tutakalo, licha ya kutia saini mikataba ya kimataifa ya kuheshimu haki za binaadamu, ikiwa pamoja na za washitakiwa, zimepita. Siku hizi nchi haziruhusiwi na hzivumiliwi ukiukaji wa haki za binaadamu au za washitakiwa.
Mtindo huu wa kuwabagua watu wa Zanzibar kwa mafungu ni wa hatari na utaiathiri Zanzibar. Fikiria serikali itahisi vipi kama watatokea watu na kusema wanaoruhusiwa kuingia katika hoteli au maduka wanayoyamiliki ni wale tu ambao sio watumishi wa serikali?
Kama serikali kupitia mahakama, ina wabagua watu kwanini na wananchi nao wasiwe na haki ya kuendeleza sera hii ya ubaguzi kwa kutumia mali zao?
Lakini kama serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar inataka kurejea tulikotoka ambapo kulikuwepo mahakama za wananchi (mahakimu wazee wanaosinzia hovyo) na kutojali uhuru wa mtu na hata kutoa hukumu kabla ya kesi kusikilizwa basi serikali isione aibu kutamka hivyo.
Kinachosikitisha ni kuona haya yanafanyika wakati Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na ile ya Mkurugenzi wa Mashitaka inaongozwa na watu wenye kuheshimika katika fani ya sheria, lakini wamekaa kimya kama vile kutoa masharti magumu au kumnyima mshitakiwa dhamana ni jambo zuri na linalofaa kupongezwa.
Nilitegemea wanasheria wenye kuheshimika kama hawa wawili wanaoongoza taasisi hizi muhimu za serikali, wangejitokeza kupinga mwenendo huu wa kibaguzi, lakini inaonekana wameweka maslahi yao mbele kuliko yale ya kulinda haki na sheria.
Wazanzibari waache utamaduni wa kulindana kwa maovu. Watu anaojiita waungwana hulindana kwa mambo mazuri na sio mabaya, hasa yale yanayoitia nchi dosari. Lakini hata jumuiya za kiraia zimekaa kimya, labda kwa kuhofia msajili kuzifuta, lakini ukweli lazima usemwe, potelea mbali liwalo na liwe.
Wazanzibari wanataka kuwa na utawala wa haki na sheria za kweli na sio bandia kama inavyojitokeza sasa.
Wazanzibari wengi walikuwa na imani na matumaini makubwa na serikali ya umoja wa kitaifa katika kusimamia haki na sheria, lakini kinachoonekana hivi sasa ni kwamba ndoto yao haikuwa ya asubuhi, mchana wala usiku.
Hakuna kitu kibaya katika nchi inayojigamba kuwa na utawala wa kidemokrasia, halafu zikaweopo dalili za vyombo vya dola na mahakama kutumika vibaya na hasa kuridhia kile kinachoonekana kama utashi wa kisiasa.
Mpaka sasa viongozi wa Uamsho hawana kosa mpaka pale itapothibitishwa bila ya wasi wasi wowote na mahakamani kuwa shutuma zinazowakabili ni za kweli na sio za kusingiziwa au kubunia.
Watu waliokabiliwa na mashitaka ya kuingiza dawa za kulevya ambazo zinaathiri maisha ya mamia ya watu, waliodaiwa kuiba mabilioni ya fedha, waliodaiwa kufanya uzemba wa meli kuzama na watu wengi kufa na wanaosemekana wameajiri wafanyakazi hewa na kuitia hasara serikali wamepata dhamana.
Ni muhimu kuelewa kwamba dunia ina tuangalia na kutucheka. Tufanye mambo mezani na kutumia hekima na busara.
Vile vile tuelewe kwamba dunia inatuangalia na hapo tutakapolaumiwa kwamba tuliziendesha mahakama zetu hovyo tusije tukasema tunaonewa.
Tujuwe kuwa hatimaye tutapanda tunachovuna, lakini historia itatukumbuka baadhi yetu kuwa tulikataa kupalilia mbegu mbaya.
Tanzania Daima

It`s time for CCM radicals to mature

BY FATMA A. KARUME
As we were catching up with some local gossip on the telephone, the only sensible way to communicategiven Dar es Salaam’s horrendous traffic congestion, a female friend of mine informed me of her absolute sadness over the death of her friend’s father.
Taken aback by her reaction, I stated, “I did not think that you were that close to the deceased”. Her calm and wistful response was “Not really, but you know the last time I met him, he said such wonderful things about my father.” It goes without saying that my friend adores her father and knowing her father I can attest that the feeling is mutual. She is no different from all the girls who have loving and doting fathers. We love to hear good things about our fathers.
Until his retirement, my friend’s father was a businessman and I very much doubt that she has ever experienced picking up a paper and reading an article penned by someone like me with a negative opinion about her father, which he wishes to air publicly; or listening to the speech of a member of the opposition aimed at annihilating any political credibility that her father may have; or worse still listening to the speech of a member of her father’s party throwing verbal missiles at her father in order to gain political mileage.
But, as the daughter of a prominent politician in Tanzania,I have experienced all of this and more. I am not writing because I want any body’s sympathy, for I understand fully that public criticism is part and parcel of a politician’s life, and actually I think it should be encouraged, hence the reason I took up the pen. What I take umbrage to are lies but even these I have lived through. There is an essential prerequisite to being the daughter of a politician and that is a thick skin. Without a thick skin, I am afraid to say, politician’s daughters would all be quivering psychological messes. Over the years, mine has metamorphosed and become as thick as the hide of an old elephant.
A week or so ago, CCM concluded its 8thCongress with much fanfare. Khadija Kopa, a taarab guru, serenaded the 2400 or so delegates, their wives and supporters all dressed in the green and yellow CCM colours and packed in a conference hall in Dodoma. There was a lot of CCM flag waving, dancing and general merry making interspersed with the serious business of choosing the new CCM office bearers from the Chairman of the party to 20 members of the National Executive Committee. The 8thCCM Congress also marked the end of AmaniAbeidKarume’s 10 years tenure as the Vice Chairman of CCM for Zanzibar. For those who are not aware, other than being the past president of Zanzibar, I like to think tongue in cheek that AmaniAbeidKarume is more famous for being my father.
On the evening of 14 November 2012, I switched on the television with the specific intent of watching AmaniAbeid Karume bid CCM his farewell as the outgoing Vice Chairman for Zanzibar. If truthis to be known I wanted to hear him thank my mother who has stood by him solidly for 44 years.
So I listened to Abraham Kinana’s pronouncement of the CCM resolutions; watched the delegates including my mother dancing to Khadija Kopa; listened to Pius Msekwa’s goodbye speech and finally Amani Karume stepped onto the podium and commenced his speech.
Karume’s farewell speech has been the most discussed and analysed speech of the 8th CCM Congress. So it is not my intention here to analyse or discuss the speech, as I am in the privileged position of knowing exactly what he meant, neither is it my intention here to defend his speech, for there have been hundreds of lines written and thousands of words spoken in support of his speech.
I seek here to analyse what I consider to be the root of the negative reaction that his speech caused in some members of CCM Zanzibar.
As I sat listening to his speech and knowing him as well as I do, I knew he was unable to conceal the happiness he felt at what he considers to be the successful conclusion of more than 10 years of service to CCM, but it was also his moment of public reflection and presentation of his parting wish list. There was nothing controversial in what he stated, for he discussed the history of CCM, the Government of National Unity in Zanzibar, the Constitutional Review Process; the responsibility of governance and good governance; and his pleasure at seeing young faces emerging in the CCM hierarchy.
In a nutshell, on the history of CCM, Karume reminded the nation that CCM is an amalgamation of two parties—the Afro Shirazi Party from Zanzibar and TANU from Tanganyika that decided to merge and consequently the ideals of its predecessors should not be forgotten, in particular ASP’s foundation policy aimed at observing the Universal Declaration of Human Rights; eradicating all forms of racial discrimination etc…
In relation to the Government of National Unity, Karume observed that this was a choice that was made by the people of Zanzibar by a 64% majority vote in a referendum, which led to an amendment of the Constitution of Zanzibar and therefore CCM must respect this choice.
With regard to the on-going Constitutional Review Process, he asked members of his party to allow people to express their views freely in particular on the question of the nature of the Union between Zanzibar and Tanganyika, and this freedom can only be exercised where authorities showed restraint.And finally, he counselled CCM that it needs to win the hearts and minds of the people, if it is to remain relevant, and this requires governance by law and humility and not through intimidation.
Frankly, I am not going to apologise for stating publicly thatAmani Karume is a man after my own heart especially given the fact that after all this he remembered to thank my mother. Having alerted you about my relationship with Amani Karume and the particular soft spot that he holds in my heart, I have discharged my duty and as we say, “caveat emptor”.
However, I was astounded with the venom with, which some members of his own party reacted to his speech. For those who follow the news will know that some CCM members were so angered by this speech that they decided to tear downKarume’s poster in Michenzani, Zanzibar.
Why should some groups within CCM in Zanzibar be so incensed by words which did nothing more than explain that the party’s mandate to govern comes from the people, and it is these people who must be respected as well as be allowed to express their views openly? I fear that this is an unfortunate consequence of the misunderstood history of CCM and our country.
On the part of Zanzibar, CCM’s predecessor the Afro-Shirazi Party came into power after a revolution and until the Constitutional Amendment of 1992, CCM’s mandate to govern Tanzania was protected by the Constitution. CCM may not have had a Godly given right to govern, but in a non-secular state, such as the United Republic of Tanzania, a Constitutional right was as close to a God given right as CCM could get. Before the amendment, article 3(1) of the Constitution of the United Republic of Tanzania used to read as follows:
“The United Republic is a democratic and socialist state which has one political party”.
No prizes for guessing, which party the “one political party” referred to in the Constitution was.
My view is that amongst some members of CCM Zanzibar, there is an unfortunate disconnect between reality and their personal beliefs and wishes.
This disconnect is emphasised by the now common site in CCM Zanzibar meetings of a group of about 50 or so ladies dressed in CCM colours who are always strategically seated by the organisers in the very front of the audience and who are then prompted like marionettes by someone to start chanting “Commando!!! Commando!!! Commando!!”.
This chant may deceive the uninitiated into believing that these ladies are die-hard supporters of Salmin Amour the CCM President of Zanzibar 1990-2000 who referred to himself as “Commando”, had no patience for the opposition,CUF, and made his impatience categorically clear by imprisoning without trial, some 20 high profile CUF members.
Of course those in the know understand the message, which the puppet masters are sending very clearly indeed. The puppet masters want a CCM Zanzibar with a “Commando” at the helm, who will handle all ‘enemies’ with the iron fist they so deserve. There are those lurking in the dark recesses of the radical wings of the party who still believe that they have an absolute right to govern because they saved Zanzibar from the Sultan and the constitutional amendments seem to have left them bewildered and rather lost in this world of competitive politics where Tanzanians get to choose which party should govern them. Well at the risk of bursting theirodd bubble those who saved Zanzibar from the clutches of the Sultan are either dead or too old and they certainly did not lead a revolution so that some opportunistic upstarts could forever entrench themselves on the Sultan’s empty thrown.
After every five years we require all political parties to put their best candidates forward and parade them before us in a bizarre beauty contest which is the hallmark of democracies the world over, and we get to pick to which beauty we hand the crown.
Lest the winner makes himself too comfortable at Ikulu either in Zanzibar or Dar es Salaam, we require him to parade himself before us five years later, when we can overlook him and proceed to pick someone else to wear the coveted crown and take the prize money.
If he is fortunate to win and wear the crown twice, as a matter of principle we must discard him at the conclusion of his 2nd term in office with a nice pension in hand of course and we move on to the next beauty. Could it be that the radicals in CCM are very aware of their inadequacies and fear that in a political beauty context, no voter will find them attractive?
To make matters more complicated, in the case of Zanzibar, the winner of the crown and the first runner up are obliged to share the prize money. Zanzibaris now expect the winner to cooperate and work hand-in-hand with his competitor. This of course requires the two previous opponents to show each other mutual respect both during the campaign trail and after the elections and to put the interests of Zanzibar first.
A fitting punishment I say, meted out in a referendum approving a Government of National Unity by 64 percent of the voting population who were clearly far too tired of the divisive politics used and abused by both CCM and CUF in Zanzibar and the tiresome and predictable cries of foul play every time we came out of an election.
Unfortunately, there are some Zanzibar CCM members who are suffering from amnesia and have conveniently forgotten the various constitutional amendments leading to the GNU; there are others who are so unused to being restrained in this manner and are restlessly champing at the bit, impatient to see the end of whatever this mass of confusion they blame AmaniAbeidKarume for allowing to take root; and there are those who have accepted the wishes of Zanzibaris and to the radicals the latter are traitors of whatever abhorrent cause they adhere to.
In a recent CCM meeting in Zanzibar, CCM radicals used abusive and racially inflammatory language reminiscent of the language used pre-revolution against none other than moderate CCM members, oblivious of the fact that the revolution was the result of race inequalities and eagerly opening past wounds in an uncouth and clumsy attempt at gaining political mileage.
As a Zanzibari of both African and Arab descent, whose Arab great grandfather was murdered in prison immediately after the revolution for nothing more than his political beliefs and whose African grandfather was assassinated 8 years after the revolution again for nothing more than his political beliefs, I am not impressed. This is a game of high stakes, which can only result in blood loss.
It is time for the radicals within CCM Zanzibar to grow up, and realise that this is not a school playground where the bully gets everyone’s lunch money.
Forty-eight years after the revolution, Zanzibar has changed irreversibly. The majority of Zanzibaris are under 40 years old. They did not live the revolution nor the divisive racial politics that led to the revolution in Zanzibar. Our politics cannot and should not remain in the past but our history should be used to inform us of where we were so that we may know where we need to go and we may learn to avoid malignant politics.
As CCM Zanzibar is being pulled by a radical wing that is becoming more prominent, so CUF is taking up the centre ground in the politics of Zanzibar. If CCM Zanzibar wants to reclaim the beauty crown in 2015, it must reform itself and fight for the centre ground because it is the votes of moderateZanzibaris that will make the next president of Zanzibar.
Ms. Karume was called to the Bar in the Middle Temple and is an advocate of the High Courts of Tanzania and Zanzibar. She is presently Litigation Partner with IMMMA Advocates in Dar es Salaam.

Wednesday 21 November 2012

Wahafidhina CCM wanapoikana misingi ya TANU, ASP

KATIKA kitabu 'Tujisahihishe' kilichoandikwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1962 ukurasa wa pili, anaeleza dhana nzima kuhusu ukweli.
Anasema, “Ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo, haujali adui au rafiki wote kwake ni sawa. Pia ukweli una tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa.
“Ukiona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa nafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya.
“Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole, japo ningekuwa nani.
“Ukweli haupendi kupuuzwa puuzwa! Wakati mwingine mtu tunayempinga huwa ana makosa kweli, lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake.
“Nikisema mbili na tatu ni sita nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nafikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha.
“Ni kweli mbili mara tatu ni sita, lakini mbili na tatu ni tano, siyo sita.
“Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema meno yangu ni machafu, au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana.
“Huu ni mfano wa upuuzi, lakini mara nyingi hoja tunazotumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda, au kukubali mawazo yetu, huwa hazihusiana kabisa na mambo tunayojadili,” anasema Mwalimu katika kitabu chake hicho.
Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume katika Mkutano Mkuu wa nane wa CCM Mjini Dodoma uliomalizika hivi karibuni analia na mtindo wa baadhi ya watu ndani ya chama kupuuzwa hata kama wanasema ukweli.
Anasema kumezuka mtindo ambao sio uliojenga misingi ya TANU na ASP wa baadhi ya watu kupuuzwa wakati wa kutoa maoni au kuchangia hoja mbalimbali, na wakati mwingine kupachikwa majina ya ajabu ambayo hayahusiani kabisa na hoja inayojadiliwa.
Karume anahimiza kuvumiliana katika utoaji wa maoni kuhusu Katiba kwani watu wamegawanyika kuhusiana na kile ambacho wanataka kiwemo katika Katiba mpya hususani suala la Muungano.

Anasema kuna watu ambao wanapendekeza Muungano uliopo udumu na wapo ambao wanataka uwe wa Serikali mbili pia kuna ambao wanapendekeza ziwe mbili lakini za mkataba.
"Wote hao ni haki yao muwastamilie, muwavumilie na wengine bungeni nimesikia wanataka Serikali tatu, si hiyari yao?" anasema Karume katika mkutano huo huku miguno na sauti za kuzomea zikianikiza katika ukumbi wa mkutano huo.
Rais huyo mstaafu wa Zanzibar hafichi hisia zake na badala yake anaeleza kuhusiana na vitendo vya wanaCCM kukosa uvumilivu wa kisiasa "uvumilivu unakushindeni hapa...! na hapa tupo wapi? Katika Mkutano Mkuu wa CCM, si mnaona?" anasema.
Anawataka wanaCCM hao wajifunze uvumilivu akiamini kuwa wanaweza, tena wanaweza vizuri sana na anawahoji iwapo maoni hayo wanakusanya wao CCM, na vipi wasiwaache waliopewa jukumu kutekeleza wajibu wao na wao kusubiri matokeo.
"Watu waachwe watu wafanya kazi yao kisha tutajua, lakini jambo la kushangaza wakitokea watu wakatoa maoni tofauti hao wanaitwa majina ya ajabu," anasema.
Anauliza vipi iwe nongwa na mtu aitwe majina ya ajabu jambo ambalo anasema sio haki wala utu na mambo kama hayo hayapo katika msingi ya TANU na ASP, vyama ambavyo vimezaa CCM.
Karume anadai kuwa Zanzibar kuna watu ambao wanawatisha wenzao kuwa mawazo yao yana lengo la kurejesha utawala wa kisultan Zanzibar.
Anasema kuwa chama hicho hivi sasa kina vijana wadogo wengi ambao hawajui kitu kuhusiana na masuala mbalimbali ya kisiasa na wanatakiwa kujifunza kwa watangulizi wao, jambo ambalo wengi hawalifanyi.
"Vijana wapya mlioingia jifunzeni kutokana na viongozi wenu waliowatangulia ili muimarishe chama chenu na matumaini ya chama chenu yapo mikononi mwenu," anasema.
Karume anasema ukweli kuwa kuna maelfu ya wanaCCM ambao ni majeruhi wa kisiasa ambao kutokana na maoni au michango yao wakati wa kujadili hoja mbalimbali likiwemo suala la Katiba.
Mifano ipo ya wahanga wa mfumo huo mbovu ndani ya chama lakini la msingi ni kuwa huyo anayesakamwa kutokana na kutoa maoni yake katika Katiba anafanyiwa hivyo kwa faida ya nani na ili iweje?
Karume ana hoja na hata wanaopingana na maoni yake wanajua hilo na hali hiyo kwa kiasi kikubwa inachagizwa na ukweli kuwa kuna wajasiriamali ambao wameijingiza katika siasa, wakiwamo vijana na hata watu wazima ambao hawajui dhana nzima ya siasa.

Pia watu hao ndio ambao hawajui chimbuko la chama wanachodai kuwa wao ni wanachama, kilipo na wapi wanaweza wakakipeleka kwani misingi ya TANU na ASP.
Misingi ya vyama hivyo inatajwa kuwa ni pamoja na pamoja na kupigania na kudumisha uhuru na raia wake.
Kulinda heshima ya kila binadamu kwa kufuata ipasavyo kanuni za tangazo la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu la Mwaka 1948 na kupinga ubaguzi wa namna yoyote na kuiwezesha nchi kuondoa ujinga, umaskini na magonjwa kwa njia ya kushirikiana.
Karume anaposema vijana wa sasa hawajui lolote anajua anachokisema kwani wanachama wanapovunja kanuni na Katiba ya chama chao kwa sababu yoyote ile ni wazi kuwa wanaofanya hivyo kwa maslahi binafsi na wala si ya umma.
Chuo cha Siasa Kivukoni au taasisi nyingine ya namna ile iwapo ingekuwepo na kutumika kama ilivyokusudiwa awali ni wazi kuwa hali ya wengine kunyooshewa vidole kutokana na kutoa maoni yao katika hoja mbalimbali ikiwemo ya Katiba isingekuwepo.
Pamoja na yote, wanaCCM na hata wanasiasa wengine lazima wakubali kuwa kila mmoja ana haki ya kuwa na maoni yake katika masuala mbalimbali, hivyo sio busara kuminywa uhuru na haki za watu ambazo zimeainishwa katika Katiba na matamko ya umoja wa mataifa.
Chanzo: Mwananchi