Monday 2 January 2012

Wahimizwa kutetea maslahi ya Zanzibar EAC

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Dk. Mwinyihaji- Makame amewataka wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) kutoka Zanzibar, kuhakikisha maslahi ya Zanzibar yanalindwa ipasavyo katika jumuiya hiyo.

Dk. Makame alisema hayo jana ofisini kwake Ikulu mjini Zanzibar wakati alipokutana na wabunge hao na kuzungumzia mambo mbalimbali ikiwemo uongozi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na uratibu wa Wazanzibari wanaoishi ughaibuni.

Katika maelezo yake, Dk. Mwinyi alisema kuwa umefika wakati kwa Zanzibar kuendelea kutambulikana na kujua nafasi yake katika jumuiya hiyo.

Alisema kuwa Zanzibar ina mengi yanayopaswa kujulikana ikiwa ni pamoja nayo kujua mengi yanayotokea na yanayoendelea katika jumuiya hiyo.

Dk. Makame alielezea anafarajika kuona wabunge hao wanafanya kazi kwa ushirikiano mazuri na wenzao kutoka nchi husika katika msimamo mmoja wa kuletea maendeleo nchi zao.

Dk. Mwinyi alisema wabunge hao kutokana na kutetea maslahi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuna haja kwa jumuiya hiyo kufanya kazi katika sehemu zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo ni Zanzibar na Tanzania Bara, ili mikakati na mipango ya
maendeleo iende sawia.

Wabunge hao akiwemo Dk. Said Kharib Bilal na Septuu Mohammed, walimueleza Waziri Makame kuwa jumuiya hiyo imekuwa ikifanya kazi zake kwa ushirikiano wa pamoja kupitia wajumbe wake kutoka nchi zote tano wanachama

No comments:

Post a Comment