Wajumbe wengi wa baraza la wawakilishi visiwani Zanzibar wametaka
Waziri wa Maji, Makaazi, na Nishari Zanzibar Juma Shamhuna ajiuzulu.
kufuatia sakata la kushirikiana kinyemela na serikali ya jamhuri ya
muungano wa Tanzania kufanikisha ombi la kutaka nyongeza ya eneo la
bahari ikijumuisha mipaka ya visiwa hivyo, pasipo kulishauri baraza
hilo.Wito wa kutakiwa kujiuzulu kwa waziri huyo mkongwe visiwani
Zanzibar unafuatia hoja binafsi iliyotolewa na mwakilishi wa Jimbo la
Mji Mkongwe Ismail Jussa. Kufutia hali hiyo Sudi Mnette alizungumza na
Issa Yusuf, Mwandishi kutoka Zanzibar kujua ni yapi yaliyojitokeza hadi
wakati huu . Tafadhali bonyeza hapa.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamemtaka waziri wa nishati zanzibar Bw
Ali Juma Shamuhuna ajiuzulu, pamoja na kupitisha azimio la kuitaka
serikali ya zanzibar kuwasilisha mara moja barua ya kupinga kitendo cha
serikali ya muungano wasilisha ombo kwa umnoja wa mataifa kuongezewa
eneo la kiuchumui katuika bahari kuu (EEZ).
Azimio hilo limefuatia hoja binafsi iliyowasilishwa na Mwakilishi wa
jimbo la Mji mkongwe Bw Ismail Jussa Ladu kuhoji uhalali wa serikali ya
muungano kuwaslisha ombi hilo UN bila kuishirika Zanzibar kikamilifu.
Katika kukabiliana na serikali ya muungano, Jussa akitoa mapendekezo
manne ambayo wajumbe wote wapiga kura kuridhia pamoja na pendekezo la
tano linaloitaka baraza la mapinduzi zanzibar kusimamia utekelezaji wa
maazimio yaliyopitishwa na baraza la wawakilishi mwezi Aprili mwaka
2009.
Mapendekezo ya Jussa ni kama ifuatayo: Kwamba seriklai ya zanzibar
inadikie serikali ya muungano barua ya kusitisha mara moja mchakato wa
maombi ya kutaka kuongezewa eneo la ukanda wa bahari kuu, na kwamba
iwapo serikali ya muungano ikipuuza serikali ya zanzibar ipeleke ujumbe
UN kutaka mchakato usimamishe.
Wiki iliyopita Serikali ya Jamhuri ya Muungano kupitia Waziri wake wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi Anna Tibaijuka iliwasilisha
maombi katika umoja wa mataifa
kuomba eneo la ziada la maili 150 nje ya eneo la sasa la maili 200 za ukanda wa kiuchumi wa eneo huru la bahari.
Katika mchakato huo serikali ya muungano ilimshirikisha waziri wa
nishati wa zanzibar Bw Ali Juma Shamuhuna kama alivyokiri mwenyewe kwa
wajumbe wenzake ndani ya baraza la wawakilishi wiki iliyopita.
“Kama waziri ni serikali, basi zanzibar ilishirikishwa, na
nilimpeleka msaidizi wangu kuniwakilisha, lakini kama serikali ni baraza
la mapinduzi, basi hakushirikishwa katika jambo hili,” Shamuhuna
alisema.
Kauli yake ilizuiwa maswali mengi kwa wajumbe wenzake miongoni mwa
maswali hayo yakiwa ni inakuwaje jambo zito kama hilo Shamuhuna
analibeba peke yake wakati baraza lilipitisha azimio linalotaka eneo
lote la bahari la EEZ pamoja na maliasli ya mafuta liondolewe katika
orodha ya muungano?
Serikali ya muungano haijajibu hadi leo kuhusu azimio la baraza,
lakini viongozi wa seriklai ya muungano wamekuwa wakitoa kauli kwamza
matatizo yote ndani ya muungano yatashughulikiwa.
Katika kuonesha kutoridhika na Shamuhuna, ndipo baadhi ya wajumbe
wakamtaka waziri huyo ajiuzulu mwenywe au rais amtimue kazi kutokana na
madai ya kuidhalilisha baraza baada ya kushirikiana na Prof Tibaijuka
kupeleka ombi UN.
“Inakuwaje waziri anakuja hapa bila ya kuwa na msimamo juu ya maswala
nyeti kama haya…waziri Shamuhuna inabidi ajiuzulu au rais amuwajibishe.
Kama hatua haitochukuliwa, tunaweza kutumia kifungu cha 41 kupiga kura
ya kutokuwa na imani na serikali…,” alisema mwakilishi Hamza Hassan Juma
(CCM Kwamtipura).
Wajumbe wengine ambao walitoa kauli za waziwazi dhidi ya Shamuhuna na
kumtaka aachiye ngazi ni Hija Hassan Hija (CUF- Kiwani), Mbarouk Wadi
Mussa (CCM- Mkwajuni), Asha bakari makame (CCM wanawake), Omar Ali Shehe
(CUF-Chakechake), na Rashid Seif Suleiman (CUF- Ziwani).
Ali Mzee Ali (CCM kuteuliwa) alitumia lugha ya kiprofesa pia kumlaumu
Shamuhuna kwamba alijitia kitanzi mwenyewe katika kuelezea ushiriki
wake katika swala ambalo bazara tayari limetolewa msimamo mwaka 2009.
Juhudi la mwanasheria mkuu wa serikali Othman Masoud kujaribu kutaka
kumkingia kifua hazikufua dafu, kwani aliposema kwamba ni mapema
kumhukumu mtu barazani alijibiwa kwa wajumbe kuguna, na baadae Jussa
kumwambia kuwa wazanzibari ambao wamekuwa wakimheshimu sana wameanza
kuvunjika moyo naye tangu alipopata wadhifa wa mwanasheria mkuu.
Hivi sasa kinachosubiriwa kwa hamu kubwa ni jibu la serikali ambalo
makamo wa pili wa rais wa zanzibar Balozi Seif ali Iddi aliahidi wiki
iliyopita kuwa katika kikao cha baraza la mapinduzi swala hilo
litazungumzwa na kujadiliwa ikiwa pamoja na kuangalia athari ya ombi la
serikali ya muungano la kutaka nyongeza ya EEZ kwa zanzibar.
No comments:
Post a Comment