Friday 13 January 2012

Tuwacheni Uvyama kwenye sherehe za kitaifa

Wafuasi wa CCM wakipita wakati wa sherehe za kutimiza miaka 48 ya mapinduza ya Zanzibar
Wafuasi wa CUF wakipeperusha bendera za chama chao kwenye sherehe hizi
Na Aby 13/12/2012
Kwa kweli huu ni utaratibu unaokera hasa katika kipindi hichi ambacho tunahitaji umoja wa Wazanzibari kuliko wakati wowote mwengine. Utaratibu huu wa kuingiza taswira za vyama katika sherehe za kiserikali inaonesha kwa kiwango gani wazanzibari hatujawa tayari kuacha tofauti zetu za kivyama na kuelekeza nguvu katika kujenga umoja ambao unahitajika kuweza kupambana na upande wa pili wa muungano katika kudai haki na maslahi ya Zanzibar iliyonyanganywa miaka 48 iliyopita.
Bali ndio kwanza tunaleta vitu ambavyo vitatugharimu kwa kiasi kikubwa, na hii zaidi inaonesha kuwa watu ambao wako katika level ya katikati kwenye vyama ndio ambao hawataki kubadilika, ukiangalia jukwaa kuu utaona viongozi wote wako neutral katika kivazi na hata ukifuatilia katika mazungumzo katika hutba zao
Haya mambo tusipokuwa makini ndiyo yatakayotupelekea kupoteza muelekeo na tukija tukipoteza mara hii basi zanzibar ndiyo itakuwa imeangamia milele, umoja unahitajika hasa tukijuwa kuwa kuna watu ndani yetu hawaipendelei Zanzibar katika kujinasuwa katika muungano usio na maslahi kwa wazanzibari, hii ilizidi kunishtuwa wiki iliyopita kuona uongozi wa juu ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa GNU unapingana kwenye jambo kubwa la maslahi ya Taifa, mmoja anasema tuwe na muungano wa serikali tatu na pia urais wa Tanzania uwe wa kupokezana badala yake mwengine kwa maslahi yake binafsi na hayo maslahi ya vyama ambayo ndiyo yaliyotufikisha hapa ana-act kinyume chake hii ni kutusaliti wazanzibari kwani nyinyi viongozi wetu tulitegemea muwe mbele katika kuungana na pia iwe ni sababu ya kutuunganisha sisi katika kudai haki ya Zanzibar katika katiba mpya.
Tunawaomba viongozi wetu wakemee suwala hili ili kwenye sherehe za kitaifa kuwe na picture sahihi ya sherehe zinazowakilisha taifa badala ya kuwa ukumbi wa kuonesha tofauti za vyama vyetu kwani vyama havikuwepo, vimekuja na baadae vitaondoka, lakini Zanzibar na wazanzibari ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo, tuwajengee misingi mizuri vizazi vyetu ili wasije wakaja kutulaumu kama sisi tunavowalaumu waliwotutangulia

No comments:

Post a Comment