Naungana na
Wazanzibari wenzangu kutoa wito kwa wazanzibari wote kuwa kitu kimoja katika
kipindi hichi ambacho Zanzibar iko kwenye msuguwano na serikali ya jamhuri ya
muungano (Tanganyika) kuhusu muswada uliopitishwa na baraza la wawakilishi
kuhusu nyongeza ya masafa ya bahari.
Kwa kweli
suwala hili limetuwekea wazi jinsi gani wenzetu watanganyika walivo na nia
mbaya na Zanzibar na jinsi gani wanavotumia mwanya wa kutugawa na kututawala,
Tumeona jinsi gani Prof. Tibaijuka alivoigeuza hoja ya wajumbe wa baraza la
wawakilishi na kuifanya ionekane kuwa ni hoja ya CUF, hii ni njia moja
wanaoyoitumia kupotosha umma wa kizanzibari kwenye mambo ya msingi kama haya.Nampongeza Mheshimiwa Hamza kwa utambuzi wake wa kulijuwa hilo na kutahadharisha mapema kuhusu njia ovu za kutugawa na kutumia udhaifu wa viongozi wetu wachache ambao hawana uzalendo na visiwa hivi na ambao wameweka maslahi yao mbele kuliko ya umma wa kizanzibari.
Hawa historia
itawakumbuka juu ya usaliti wao dhidi ya Wazanzibari, na akina hamza na Jussa
pia pia nao historia itawakumbuka na kuwaenzi
kwani historia inaonesha wale wote ambao wanakuwa upande wa umma ndio
ambao hufanikiwa katika mbio zao kwenye nyanja mbali mbali ikiwemo za kisiasa.
Mwisho
napendekeza Wazanzibari tuwe na utamaduni wa kuonesha hisia zetu kwenye mambo
muhimu kama haya ili kwa hatuwa hizo tutakuwa tunawapa nguvu na kujiamini wale
viongozi wetu ambao wanatetea maslahi yetu, nimeona hatuwa nyingi zinachukuliwa
na sisi ambao tuko kwenye hii mitandao ambayo coverage yake ni ndogo sana mimi
ningependekeza wale ambao wako nyumbani tuwe na utamaduni hata wa kuitisha
maandamano locally kuwaunga mkono hawa viongozi wetu kwa mfano siku ambayo
wanajadili hoja muhimu kama hizi tunapaza sauti zetu hata pale nje ya baraza la
wawakilishi.
No comments:
Post a Comment