Kikao cha kamati ya pamoja ya serekali ya Muungano wa Tanzania na
Serekali ya Zanzibar kimekutana chine ya Mwenyekiti wake Makamu wa Rais
wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Mohd Gharib Bilali.
Kikao hicho kilicho husisha Mawaziri,makatibu Wakuu,Watendaji wa
Serekali Wakiwemo pia Wataalamu Kilifanyika kwenye ukumbi wa Blue Ubungo
Plaza Mjini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Kikao hicho walikubaliana kuthibitisha kumbu kumbu za
kikao cha Kamati ya pamoja ya SMT na SNZ cha Tarehe 2 Juni mwaka 2010
kilichokutana Bwawani Mjini Zanzibar.
Halkazalika Wajumbe hao walipitia Taarifa ya utekelezaji wa
yatokanayo na Kikao hicho ambayo ni ushiriki Zanzibar katika jumuiya ya
Afrika Mashariki, Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia,Uvuvi
katika ukanda wa Bahari kuu na Ushirikiano wa Zanzibar katika Tasisi za
nje.
Tarifa nyingine ni ajira kwa watumishi wa Zanzibar katika tasisi za
Muungano, Mgawanyo wa mapato na faida yatokanayo na Bank kuu ,
Malalamiko ya wafanya biashara kutozwa kodi mara mbili waingizapo pidhaa
zao Tanzania Bara,usajili wa vyombo vya moto, likiwepo pia ongezeka la
gharama za Umeme wa Tanesco kwenda ZECO uharamia na utekaji nyara meli.
Katika majadiliano hayo Mwenyekiti wa kikao hicho Dr Mohd Gharib
Bilal aliagiza mamlaka zinazo husika kutowa maelezo ndani ya kipindi cha
miezi mine utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asilia.
Mapema mwana sheria mkuu wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh.
Othmani Masoud Othman Taratibu zote na Baraka kuhusu swala hilo
zimeshachukuliwa na Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Baraza la
Mapindizi na Baraza la Wawakilishi na kuliwakilisha Serekali ya Muungano
kwa hatuwa za kisheria.
Naye makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
alisisitiza hoja ya kuwa na ratiba malum ya vikao pamoja na kupunguza
urasimu wa utekelezaji wa mamuzi yanayofikiwa katika vikao hivyo vya
pamoja.
Balozi Seif alisema itapunguza kero zilizopo na hatimae kuamsha ari ya kuimarisha Muungano kwa pande zote mpili.
Nirahisishieni kazi ndani ya Baraza la Wawakilishi kwa wajumbe wake
wako Solidarity na hakuna mjumbe wa CCM wala CUF katika swala lolote
linalohusu Muungano,alisisitiza Balozi Seif.
Katika kikao hicho upande wa wajumbe wa Serekali ya Muungano
uliongozwa na Waziri mkuu Mh. Mizengo Peter Pinda wakati ule wa Zanzibar
uliongozwa na makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi seif Ali Iddi.
No comments:
Post a Comment