Tuesday 31 January 2012

Vikao vingi utekelezaji Zero

Kikao cha kamati ya pamoja ya serekali ya Muungano wa Tanzania na Serekali ya Zanzibar kimekutana chine ya Mwenyekiti wake Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Mohd Gharib Bilali.
Kikao hicho kilicho husisha Mawaziri,makatibu Wakuu,Watendaji wa Serekali Wakiwemo pia Wataalamu Kilifanyika kwenye ukumbi wa Blue Ubungo Plaza Mjini Dar es Salaam.
Wajumbe wa Kikao hicho walikubaliana kuthibitisha kumbu kumbu za kikao cha Kamati ya pamoja ya SMT na SNZ cha Tarehe 2 Juni mwaka 2010 kilichokutana Bwawani Mjini Zanzibar.
Halkazalika Wajumbe hao walipitia Taarifa ya utekelezaji wa yatokanayo na Kikao hicho ambayo ni ushiriki Zanzibar katika jumuiya ya Afrika Mashariki, Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia,Uvuvi katika ukanda wa Bahari kuu na Ushirikiano wa Zanzibar katika Tasisi za nje.
Tarifa nyingine ni ajira kwa watumishi wa Zanzibar katika tasisi za Muungano, Mgawanyo wa mapato na faida yatokanayo na Bank kuu , Malalamiko ya wafanya biashara kutozwa kodi mara mbili waingizapo pidhaa zao Tanzania Bara,usajili wa vyombo vya moto, likiwepo pia ongezeka la gharama za Umeme wa Tanesco kwenda ZECO uharamia na utekaji nyara meli.
Katika majadiliano hayo Mwenyekiti wa kikao hicho Dr Mohd Gharib Bilal aliagiza mamlaka zinazo husika kutowa maelezo ndani ya kipindi cha miezi mine utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asilia.
Mapema mwana sheria mkuu wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh. Othmani Masoud Othman Taratibu zote na Baraka kuhusu swala hilo zimeshachukuliwa na Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Baraza la Mapindizi na Baraza la Wawakilishi na kuliwakilisha Serekali ya Muungano kwa hatuwa za kisheria.
Naye makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisisitiza hoja ya kuwa na ratiba malum ya vikao pamoja na kupunguza urasimu wa utekelezaji wa mamuzi yanayofikiwa katika vikao hivyo vya pamoja.
Balozi Seif alisema itapunguza kero zilizopo na hatimae kuamsha ari ya kuimarisha Muungano kwa pande zote mpili.
Nirahisishieni kazi ndani ya Baraza la Wawakilishi kwa wajumbe wake wako Solidarity na hakuna mjumbe wa CCM wala CUF katika swala lolote linalohusu Muungano,alisisitiza Balozi Seif.
Katika kikao hicho upande wa wajumbe wa Serekali ya Muungano uliongozwa na Waziri mkuu Mh. Mizengo Peter Pinda wakati ule wa Zanzibar uliongozwa na makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi seif Ali Iddi.

No comments:

Post a Comment