Saturday 31 December 2011

SMZ macho kuimarisha huduma za jamii- 2012

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), mwaka huu imeahidi kuendelea kuimarisha miundombinu na ubora wa huduma za jamii zikiwemo elimu, afya na maji safi na salama.
Hayo yalisemwa jana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali
Mohamed Shein katika risala yake ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2012, aliyoitoa Ikulu,
mjini hapa.
Aidha katika risala yake, Dk. Shein alieleza kuwa katika mwaka 2012, Serikali itaongeza
ushirikiano na sekta binafsi ili kwa pamoja kufikia lengo la kukuza uchumi na kupunguza
umasikini.
Katika kukabiliana na athari za uchumi wa dunia hususan ongezeko la bei ya chakula alisema
serikali itaimarisha sekta ya kilimo.
Akieleza mipango ya kiuchumi kwa mwaka 2012 Dk. Shein alisema kuwa Serikali inaazimia
kuzidi kuongeza ukusanyaji wa kodi na kuimarisha mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia
wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Dk. Shein alisisitiza kuwa katika kuelekea mwaka 2012 kuna mambo muhimu ya
kuyazingatia na kuyatekeleza ipasavyo kwa ustawi wa maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na
kuimarisha amani na utulivu
Chanzo: Habari leo

No comments:

Post a Comment