Aliyasema hayo alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tathmini ya mwaka mmoja tangu
kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) Novemba, mwaka jana.
Akitoa mfano Maalim Seif
alisema Hoteli ya Zanzibar Ocean View, imejengwa katika eneo ambalo kwa
mujibu wa wataalamu wa mazingira, haliruhusiwi kuanzishwa kwa ajili ya
mradi huo.
Alisema anashangaa kwamba
hata baada wataalamu kuzuia eneo hilo kwa mradi huo, hoteli hiyo
ilijengwa baada ya wamiliki kubebwa na viongozi wazito serikalini.
Mfano mwingine wa uvunjaji
wa sheria za mazingira alisema ni ujenzi wa hoteli ya kitalii ya Misali
ambayo imejengwa kinyume na Sheria za Uhifadhi wa mazingira kisiwani
Pemba.
Alisema hoteli hiyo
imejengwa karibu na kituo cha kuhifadhi mafuta ya aina mbalimbali pia
karibu na Kituo cha umeme cha Wesha ambacho hupokea nishati hiyo kutoka
gridi ya taifa kupitia waya uliotandikwa chini ya bahari kuanzia mkoani
Tanga.
Maalim Seif alisema hata
wataalamu wa mazingira wanaposhauri miradi inayokiuka uhifadhi wa
mazingira ivunjwe maamuzi yao yamekuwa hayazingatiwi kutokana na
wawekezaji hao kulindwa na vigogo serikalini.
Alisema kitendo hicho ni
cha hatari kwa sababu kina hatarisha usalama wa wananchi na mpango mzima
wa uhifadhi wa mazingira pamoja na kwenda kinyume na misingi ya utawala
wa sheria.
Alisema wapo wawekezaji
ambao wamediriki kujenga ndani ya fukwe za bahari tofauti na maelekezo
ya kisheria kwamba miradi kama hiyo ijengwe umbali wa mita 30 kutoka
ufukwe wa bahari.
Alisema kitendo cha baadhi
ya viongozi kuwaruhusu wawekezaji kuvunja sheria hatimaye kitakuwa na
madhara katika suala la kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Alisema licha ya
kuhatarisha uhifadhi wa mazingira, ujenzi vitenga uchumi fukweni pia
umeibua migogoro mikubwa kati ya wavuvi wadogo wadogo na na wawekezaji
walioanzisha miradi yao katika fukwe.
Aidham alisema wakati
umefika kwa wananchi wa kuongeza uwajibikaji katika kulinda na kuhifadhi
mazingira hasa kwa kujiepusha na vitendo vya ukataji miti ya mikoko,
uchimbaji wa mchanga na matumizi mabaya ya fukwe za bahari.
Alisema katika kupambana na
tatizo la uchafuzi wa mazingira ikiwemo kudhibiti matumizi ya mifuko ya
plastiki, serikali imeunda kamati maalum ya kuwasaka wanaoingiza mifuko
hiyo kutoka nje ya nchi na wanauza kwa wananchi kwa rejareja.
Hata hivyo, alisema adhabu
ya faini ya Sh. milioni 10 kwa mtu anayepatikana na kosa la kuwa na
mfuko mmoja wa plastiki na Sh. milioni 10 kwa mtu anayetiwa hatiani kwa
kuwa na shehena ya mifuko hiyo inahitaji kuangaliwa upya utekelezaji
wake.
Alisema kwa msingi huo serikali imeamua kuiangalia upya sheria hiyo kabla ya kuanza kuwakamata wananchi wanaotumia mifuko hiyo na kuwafikisha mahakamani kutokana na kuwa tayari imepigwa marufuku matumizi yake
Chanzo: Nipashe
No comments:
Post a Comment