Friday 17 February 2012
Tangazo muhimu la mijadala ya mustakbali wa nchi yetu - Zanzibar
Inshaallah Kesho Jumamosi asubuhi saa 2.30 katika ukumbi wa Beit Al
Yamin Malindi kutakuwa na mjadala wa wazi wa wadau wote wa elimu kuhusu
matokeo ya mtihani wa taifa kidato cha nne. Mjadala huo utawashirikisha
walimu wa skuli za serikali na binafsi, wazazi, wanafunzi na wadau
wengine wa elimu karibuni katika mjadala huo ili kutoa maoni yenu katika
mjadala huo. Aidha Kesho hiyo hiyo jioni
inshallah saa 4:30 eneo la Mapembeani Mwembe Tanga kutakuwa pia na
mkutano wa kutoa elimu ya uraia kuhusu katiba, mkutano ambao umeandaliwa
na baraza la katiba zanzibar mnaombwa kuhudhuria kwa wingi katika
mkutano huo, vitabu vya KATIBA TUITAKAYO vitatolewa bure katika mkutano
huo. watakaoongoza utoaji wa elimu ni pamoja na Professa Abdul Shareef,
Awadh Said na Ally Saleh. Mnakaribishwa kuhudhuria kwa wingi na mnaombwa
kwa kila atakayesikia tangazo hili amuarifu na mwenzake
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment