Friday 10 February 2012

Matokeo ya mitihani F4 ni janga la Taifa Zanzibar

Kwa kweli hili ni janga kwa mustakbali wa elimu ya Zanzibar, Nahisi tatizo ni kuwa kuna mtiririko mrefu wa masuali ya kujiuliza na pia wahusika ambao wanahitajika watiwe hatiani kabla ya hao watoto kufutiwa matokeo.

1. Baraza la mitihani lenyewe inakuwaje mitihani ivuje, definitely wao ndio ambao wanavujisha mitihani
2. kama mitihani imefutwa kwa wanafunzi, mfano Haile salasie hakuna wasiwasi kwa mazingira ya Zanzibar lazima Ben bela nao watapata, so kama kufutiwa wafutiwe wote.
3. Ndalichako anajitetea tuu ila madudu yote yako huko baraza la mitihani ambako wanavujisha mitihani kwani haiwezekani pia mitihani ivuje Zanzibar wakati baraza la mitihani liko Dar.
4. Hapa mitihani inahitajika irudiwe kwani mbona wao mitihani ya darasa la saba wameirudia kwa sababu walifkiria mustakbali wa watoto wao so na sisi pia kwa kuzingatia maslahi ya vijana wetu mitihani irudiwe. 


Then Serikali ya Zanzibar ishikie bango baraza la mitihani libebe jukumu lote la madudu yaliyotokea badala ya kuunda tume zisizokuwa na maana wala hatuoni result zake au tujipange tutengeneze baraza letu hilo linawezekana pia.

No comments:

Post a Comment