Tuesday 13 March 2012

Wanaosaka ajira Oman wakwama Zanzibar

ZAIDI ya vijana 150 waliokuwa wasafirishwe kwenda Oman kwa ajili ya kupata ajira katika viwanda mbalimbali, wamekwama baada ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kushindwa kuitambua Kampuni ya Zam Agency yenye makao makuu yake Unguja, inayowasafirisha vijana hao.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Zainab Ramadhan Mohammed aliwaambia waandishi wa habari kwamba kampuni yake imekwama kusafirisha vijana hao ambao walikuwa waende Oman kufanya kazi katika viwanda mbalimbali, baada ya kukamilika kwa masharti mbalimbali ikiwemo mikataba halali ya ajira.
“Tunasikitika sana kusema tumeshindwa kusafirisha vijana 150 ambao walikuwa waende Oman kufanya kazi katika kampuni za viwanda ikiwemo vya kutengeneza maziwa kwa sababu Serikali haijakubaliana na sisi ikiwemo kutupa kibali cha kufanya kazi hiyo,” alisema Zainab.
Zainab alielekeza shutuma zake kwa Waziri wa Kazi, Maendeleo ya Vijana na Ushirika, Haroun Ali Suleiman ambaye alizungumza katika vyombo vya habari akisema kwamba kampuni yake haitambui.
Alisema alisikitishwa na kauli hiyo ya waziri kwa sababu kampuni yake imesajiliwa na kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo za kutoa misaada ya kibiashara.
Alisema kutokana na uamuzi wa SMZ kuchelewesha kutoa kibali kwa kampuni hiyo, tayari ajira 200 zimepotea na kuchukulia na Serikali ya Kenya iliyopeleka watu kufanya kazi katika kampuni na sehemu za viwandani.
Alisema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho za kumuona tena waziri ili kulipatia ufumbuzi suala hilo ikiwemo kutoa kibali cha ruhusa ya kusafirisha vijana nje ya nchi ili kupata ajira zenye kutambulika rasmi.
Zainab alionesha mkataba wa kusafirisha vijana kwenda Oman wa Kampuni ya Ilya Manpower ambao unatakiwa kujazwa na wizara husika ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Hivi karibuni, Waziri Haroun alipozungumza na waandishi wa habari alizitaka kampuni ambazo hazina vibali, kuacha kusafirisha vijana nje ya nchi

No comments:

Post a Comment