ZAIDI ya vijana 150 waliokuwa wasafirishwe kwenda Oman kwa ajili ya
kupata ajira katika viwanda mbalimbali, wamekwama baada ya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kushindwa kuitambua Kampuni ya Zam Agency
yenye makao makuu yake Unguja, inayowasafirisha vijana hao.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Zainab Ramadhan Mohammed
aliwaambia waandishi wa habari kwamba kampuni yake imekwama kusafirisha
vijana hao ambao walikuwa waende Oman kufanya kazi katika viwanda
mbalimbali, baada ya kukamilika kwa masharti mbalimbali ikiwemo mikataba
halali ya ajira.
“Tunasikitika sana kusema tumeshindwa kusafirisha vijana 150 ambao
walikuwa waende Oman kufanya kazi katika kampuni za viwanda ikiwemo vya
kutengeneza maziwa kwa sababu Serikali haijakubaliana na sisi ikiwemo
kutupa kibali cha kufanya kazi hiyo,” alisema Zainab.
Zainab alielekeza shutuma zake kwa Waziri wa Kazi, Maendeleo ya
Vijana na Ushirika, Haroun Ali Suleiman ambaye alizungumza katika vyombo
vya habari akisema kwamba kampuni yake haitambui.
Alisema alisikitishwa na kauli hiyo ya waziri kwa sababu kampuni
yake imesajiliwa na kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo za kutoa misaada
ya kibiashara.
Alisema kutokana na uamuzi wa SMZ kuchelewesha kutoa kibali kwa
kampuni hiyo, tayari ajira 200 zimepotea na kuchukulia na Serikali ya
Kenya iliyopeleka watu kufanya kazi katika kampuni na sehemu za
viwandani.
Alisema kwa sasa wapo katika hatua za mwisho za kumuona tena waziri
ili kulipatia ufumbuzi suala hilo ikiwemo kutoa kibali cha ruhusa ya
kusafirisha vijana nje ya nchi ili kupata ajira zenye kutambulika rasmi.
Zainab alionesha mkataba wa kusafirisha vijana kwenda Oman wa
Kampuni ya Ilya Manpower ambao unatakiwa kujazwa na wizara husika ya
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Hivi karibuni, Waziri Haroun alipozungumza na waandishi wa habari
alizitaka kampuni ambazo hazina vibali, kuacha kusafirisha vijana nje ya
nchi
No comments:
Post a Comment