Friday 2 March 2012

Mradi Mkubwa Bandari Lamu wazinduliwa

Ujenzi wa mradi mkubwa wa bandari na utakaogharimu $23bilioni (£14.5bn) kusini mashariki mwa pwani yaKenyakatika mji wa Lamu karibu na mpaka wa Somalia umezinduliwa.
Bomba la mafuta, reli na barabara pia zitajengwa kuunganisha Lamu na Sudan Kusini na Ethiopia.
Nchi iliyopata uhuru wake hivi karibuni ya Sudan Kusini ina mipango ya kutumia Lamu kama njia kuu ya kusafirishia mafuta yake.
Mwandishi wa BBC anasema wasiwasi kuhusu usalama wa mradi huo unaweza kuelezea umhimu wa kuwepo kwa vikosi vyaEthiopianaKenyanchiniSomaliavikilenga kulipatia utulivu eneohilo.

'Mradi mkubwa zaidi Afrika'

Rais wa Kenya Mwai Kibaki alizindua mradi huo sambamba na Rais wa Sudan Kusini na Waziri Mkuu waEthiopiaMeles Zenawi.
"Sina mashaka kuwa siku hii itakumbukwa katika historia wakati tunapojaribu kuwaunganisha watu wetu na kupata fursa za muhimu za kiuchumi na kijamii kwa ajili ya maishayaoyajayo" Shirika la habari la AFP limemnukuu Rais Kibaki akisema wakati wa sherehe za uzinduzi.
Ikifahamika kama kama Bandari ya Lamu ya usafiri ukanda wa Sudan KusiniEthiopia(Lapsset), inatarajiwa kumalizika kwa miaka minne ikiwa na gharama za awali kutoka serikali hizo tatu huku mipango ya kuwaalika wawekezaji wa kimataifa ikiwekwa.
Steven Ikuwa, anayesimamia mradi huo aliiambia BBC kuwa mipango hiyo ni mikubwa.
"Nina furaha kusema kuwa huu ni mradi mkubwa kabisa ambao tunauanza barani Afrika."
Mwandishi wa BBC Noel Mwakugu akiwa Lamu anasema kuna wasiwasi kuhusu mazingira ya eneo la mradi huo ambalo ni sehemu zuri zaidi kimazingira Afrika Mashariki sambamba na bahari ya Hindi na utajiri wa urithi wa kimazingira katika kisiwa cha Lamu.
"Lamu ni urithi ulio hai. Tayari Unesco imetangaza Lamu kuwa Urithi wa Dunia na kuwa eneo lililo katika hatari ya kupotea," Mualimu Badi kutoka kundi la Save Lamu aliiambia BBC.
"Iwapo watu 500,000 watakuja hapa kama wafanyakazi nadhani tutapoteza hadhi hiyo. "
Bw Badi pia alisema wenyeji wana wasiwasi wa kukosa makazi kutokana na kutokuwa na uthibitisho kuwa ni wakazi halali wa eneo hilo.
Akijibu malalamiko hayo Rais Kibaki ametangaza kuwa wakazi wa eneo hilo watapewa hati za kumiliki ardhi na utawala wake utatoa mafunzo kwa vijana 1,000 kuwaandaa kwa fursa zitakazotokana na bandari hiyo.
Chanzo: BBC

No comments:

Post a Comment