“Wakati tunaelekea India wiki iliyopita tukiwa Uwanja wa Ndege wa Dubai
wakati tunabadilisha ndege, tulikutana na mmoja wa Makamishna wa Tume ya Katiba
kutoka upande wa Tanganyika ambaye ni msomi wa hali ya juu.
Katika majibu ya kustaajabisha wakati nilipomuuliza vipi hali ya utoaji maoni
inaendelea, alitujibu kuwa inaendelea vizuri na pamoja na kwamba upande mmoja
(nna hakika alikusudia Zanzibar) unatoa madai makubwa, yeye haimpi tabu kwa
sababu anajua wanaofanya hivyo wanajipa nafasi kubwa ya kuja kupatana (alitumia
neno la Kiingereza ‘bargaining’) ili kupata muafaka wa kati na kati.
Bahati mbaya mawazo kama haya ya Kamishna huyu ndiyo mawazo mgando ya watunga
sera na sheria wengi wa Tanganyika wanaojiona kama ni watawala au wamiliki wa
Zanzibar na hivyo kujipa matumaini kuwa Zanzibar tunaposema tunataka kurejesha
mamlaka yetu kamili kitaifa na kimataifa tukiwa na kitu chetu Umoja wa Mataifa
huwa tunatafuta ‘kupatana’ au kwamba hatuna uwezo huo mpaka Tanganyika waridhie.
Wanapaswa wajue sasa kabla hawajachelewa kwamba mamlaka kamili ya Zanzibar
(Sovereign Zanzibar) siyo ombi ni matakwa ya Wazanzibari na tutayasimamia kwa
nguvu na uwezo wetu wote. Na katika kulifikia lengo hilo hakuna wa kutuzuia
isipokuwa Mwenyezi Mungu. Pamoja Daima!”
JUSSA @FACEBOOK WALL.
No comments:
Post a Comment