Friday 1 February 2013

Ukivunjika muungano nini Kitatokea?


Hoja za Watetezi wa Muungano
1. Muungano ukivunjika Wapemba walio na maduka dar watarudi kwao
  Huu ni upotoshaji kwani kuna wachina wanauza hadi karanga, jee kuna muungano wa china na Tanganyika?
2. Wazanzibari na Watanganyika wameowana
  Hii ni hoja ya pili ambayo pia haina mashiko, Wazanzibari na Watanganyika wameowa wazungu na wachina jee kuna muungano na nchi hizo, Mzee wetu (Mpigania haki Maarufu za wazanzibari) Nassoro Moyo aliowa mtanganyika mwaka 1951, jee kulikuwa na muungano wakati huo.
3. Wazanzibari tukivunja muungano tutakosa kununuwa vitunguu na mbatata tanganyika,
  Tunafanya biashana na nchi mbali mbali Africa na ulaya na Asia jee kuna muungano na nchi hizo.
4. Wanaodai muungano wa mkataba au uvunjike wanataka kumleta muarabu
  Huu ndio kabisa sio akili bali matope, nimezaliwa miaka ya sabiini, sijui habari za mfalme wala upumbavu gani nahitaji Zanzibar yangu yenye mamlaka kamili.
5. Wazanzibari tutagawanyika uunguja na Upemba
    Zanzibar ilikuwepo kabla ya Muungano, jee kuna muungano wa Unguja na Pemba?
6. Tunaihitaji Tanganyika kwa ajili ya ulinzi
     hii ni kututia woga ila kuna nchi ndogo kuliko Znz na zina ulinzi imara, jeshi letu la Zanzibar lilikuwa strong kabla ya muungano, baada ya muungano ndio tumefika tulipo.

Next time nitaeleza faida kwa nini tunahitaji Zanzibar mamlaka kamili

No comments:

Post a Comment